Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, October 8, 2015

MAADHIMISHO YA SIKU YA MTINDIO WA UBONGO DUNIANI KITAIFA YAFANYIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwenyekiti wa Chama cha Wazazi wa Watoto Wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo Tanzania (Chawaumiviata), Hilal Said wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho ya Siku ya Mtindio wa Ubongo Duniani yaliyoadhimishwa viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana.
 Mzazi mwenye mtoto mwenye changamoto ya maradhi hayo, Titus Chengula akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho hayo.
Mzazi  Ester Peter kutoka Makuburi eneo la Ubungo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu changamoto walizonazo kuwalea watoto wenye matatizo hayo.

 
 Wanachama wa Chama cha Wazazi wa Watoto Wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo Tanzania (Chawaumiviata), wakiwa na viongozi wao kwenye Maadhimisho ya Siku ya Mtindio wa Ubongo Duniani yaliyofanyika hapa nchini kitaifa viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana.
 Mama akimsaidia mtoto wake kutembea katika maadhimisho hayo.
 Hapa wakiwa katika picha ya pamoja.
 Burudani zikiendelea.
Picha zikipigwa na mmoja wa wafadhili wao

Na Dotto Mwaibale

WAKUU wa Shule mbalimbali wametakiwa kuwapokea watoto wenye mtindio wa ubongo kujiunga na darasa la kwanza badala ya kuwakataa kwa maelezo shule zao hazina walimu maalumu wa kuwafundisha.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Chama cha Wazazi wa Watoto Wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo Tanzania (Chawaumiviata), Hilal Said wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho ya Siku ya Mtindio wa Ubongo Duniani yaliyoadhimishwa viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana.

"Changamoto kubwa waliyonayo watoto wenye utindio wa ubongo hapa nchini ni kukataliwa na wakuu wa shule mbalimbali pale wanapokwenda kuandikishwa darasa la kwanza kwa madai ya shule hizo kutokuwa na walimu wa kuwafundisha" alisema Said.

Said alisema walimu hao wanapaswa kuwapokea watoto hao badala ya kuwakataa jambo litakalo wafanya wajione hawanyanyapaliwi.

Alisema baadhi ya walimu wamekuwa wakiwaeleza wazazi wao kuwa wawapeleke watoto hao katika shule maalumu zenye walimu ambazo pia haziwasaidii watoto hao kwa kuwa wakiwa katika shule hizo wanakuwa ni watoto wenye matatizo yanyofanana.

Said alisema kuwachanganyanga watoto hao na watoto wengine katika shule za kawaida inawasaidia kuwachangamsha na kujiona kama walivyo wenzao.

Mmoja wa wazazi wa mtoto mwenye matatizo hayo Ester Peter kutoka Makuburi eneo la Ubungo alisema maadhimisho kama hayo yamekuwa yakiwakutanisha wazazi na watoto wao wenye matatizo hayo ambapo ubadilishana mawazo ya namna ya kuwalea watoto hao na kupata ushauri kutoka kwa wataalamu.

Mzazi mwingine Titus Chengula kutoka Ubungo External alisema wazazi wenye watoto wenye matatizo ya afya wasiwafungie ndani badala yake wawasaidi na kuwapekeka shule na vituo vinavyo wasaidia katika mazoezi ya viungo.
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

No comments:

Post a Comment