Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, November 6, 2015

LOWASSA Afunguka Kuhusu Ujio wa TB JOSHUA Kuja Kumuona..Atoa Kauli Nzito

Nashukuru kwa heshima aliyonipa mtumishi wa Mungu, T.B Joshua kwa kuja nyumbani kujadili mambo ya taifa, na baadaye kushiriki kwenye sala na ndugu na familia. Mungu atuongoze. Mungu ibariki Tanzania!"-Edward Ngoyai Lowassa
Maelezo kwa mujibu wa tovuti ya John Kitime (johnkitime.co.tz)Temitope Balogun Joshua (T.B. Joshua) alizaliwa tarehe 12 Juni 1963, katika kijiji kidogo cha Arigidi kilichoko Akoko, Jimbo la Ondo, Nigeria. Inasemekana mama yake alikaa na mimba kwa miezi 15, kabla Temitope hajazaliwa.

Katika kabila lake kulikuweko na hadithi ya zaidi ya miaka 100 ambayo ilitabiri kuwa kuna mtoto atazaliwa katika familia masikini, ambaye Mungu atamtumia sana, na wengi kule kwao huamini kuwa Temitope ndie aliyetajwa katika utabiri huo. Siku tatu baada ya kuzaliwa kwake, jiwe kubwa lilirushwa kutoka kwenye sehemu kulikokuwa kunapasuliwa mawe, jiwe hilo lilitoboa bati na kumkosa kosa Temitope kwa sentimita chache. Na ndipo mama yake alimpa jina la Temitope, likiwa na maana ‘Ulichonipa Mungu lazima kishukuriwe’.
Jina analojulikana sana sasa ni T. B. Joshua.


TB Joshua ni muhubiri mwanzilishi na kiongozi wa The Synagogue, Church of All Nations (SCOAN), hii ni taasisi ya kidini inayoendesha Emmanuel TV, Tv ambayo huonekana kote duniani ikiwa inarushwa kutoka Lagos Nigeria. TB Joshua anasemeka ni moja ya watu 50 wenye ushawishi zaidi Afrika, anajulikana sana kwenye mitandao ya Facebook ambako anawafuasi zaidi ya milioni moja laki tano, na video zake nyingi zilizomo kwenye Youtube. Kwa mujibu wa Forbes, mwaka 2011 TB Joshua alikuwa mtu wa tatu kwa utajiri nchini Nigeria.

Wakati akiwa shule alijulikana kwa jina la Balogun Francis, alisoma shule ya St. Stephen’s Anglican Primary School ya Arigidi-Akoko, kati ya mwaka 1971 na 1977, lakini hakumaliza sekondari. Wakati yuko shule alijulikana kama “small pastor” kutokana na kupenda sana biblia, baada ya kuacha shule alifanya kazi mbalimbali ndogo ndogo, hatimae akaanzisha darasa la biblia kwa watoto, wakati huohuo akaanza kujiendeleza kwa masomo ya jioni. Hatimae akaamua kwenda kujiunga na jeshi la Nigeria, lakini kwa bahati mbaya akaachelewa treni kwenda kwenye usaili na hivyo ndoto hiyo ikaishia hapo.

Kwa maelezo yake mwenyewe anaeleza jinsi alivyokabithiwa upako wake, “ Nilikuwa katika hali ya kuzimia kwa siku tatu mfululizo, nikaona mkono ukielekeza Biblia kwenye moyo wangu, na Biblia ikaingia kwenye moyo wangu na moyo wangu wa zamani ukachanganyika na Biblia. Ufahamu uliponijia nikawaona Mitume na Manabii wa zamani wako na mtu ambaye sikuweza kuona kichwa chake kwa sababu alikuwa mrefu sana amefika mpaka mbinguni. Nikaamini kuwa alikuwa ndie Bwana wetu Yesu Kristo, nami nikajiona nimo katika hawa Manabii na Mitume wa zamani.
Nikauona mkono wa yule mtu mrefu sikuweza kuona uso wake maana ulikuwa na mwanga mkali sana sikuweza kabisa kuangalia uso wake. Lakini Mitume wengine niliweza kuwaona. Mitume Peter na Paul, Manabii Moses, Eliya na wengine, kwani majina yao yalikuwa yameandikwa kwa herufi kubwa vifuani mwao. Nikasikia sauti inasema, “Mimi ni Mungu wako, nakupa upako nenda kafanye kazi ya baba yako wa mbinguni.”
Wakati huohuo yule mtu mrefu akanipa Msalaba na Biblia iliyokuwa kubwa kuliko ile iliyoingia moyoni mwangu. Akaniahidi kuwa kila nitakapo tumia muda wake na jina lake nitapata Msalaba mkubwa zaidi, nikienda kinyume na mambo yatakuwa kinyume. Nikasikia sauti ya yule mtu mrefu ambaye sikuwa naweza kuona kichwa chake ikasema,’ Mimi ndie Bwana wako, niliyekuwa na ambaye ndie, mimi ni Yesu Kristo ninaetoa amri kwa mitume na manabii wote. Sauti ile ikasema tena ‘Nitakuonyesha mambo mazuri ya ajabu na nitajionyesha kupitia mafunzo, mahubiri, miujiza, ishara, kwa ajili ya kuokoa roho za watu. Kutoka wakati huo nimekuwa napata maono kila mwaka na Msalaba mkubwa zaidi ukiwa na maana majukumu makubwa zaidi”

SCOAN ina tawi moja tu nalo liko Ghana, kwa sasa kila Jumapili kuna ibada Nigeria ambayo huhudhuriwa na kiasi cha watu 15,000 kila Jumapili. Uponyaji ni kati ya mambo mengi yanayofanywa katika kanisa la TB Joshua watu wengi wamekuwa wakisema wamepona maradhi mbalimbali kutokana na kufika kanisani hapo na kwa kutumia maji, ‘annointed water’ ambayo hutolewa na TB Joshua.
Wakati wa tatizo la Ebola TB Joshua alisema maji hayo yanaweza kutibu ugonjwa huo na alituma chupa 4,000 za maji hayo zikiambatana na dola 50,000 kwenye serikali ya Sierra Leon. Hili lilikuja hasa baada ya maafisa afya wa Lagos walipomtembelea TB Joshua kumtaka asiwaruhusu wagonjwa Ebola kuja katika kanisa hilo kwa kuondoa uwezekanao wa kupata mlipuko wa ugonjwa huo katika jiji hilo. Wasanii wa Nollywood kama Jimmy Iyke na Camilla Mberekpe pia ni kati ya watu wengi waliowahi kupata huduma za kuondoa mapepo katika miili yao katika kanisa hilo.

Pia TB Joshua anasemekana ameweza kutabiri mambo mengi ikiwemo kifo cha Michael Jackson, milipuko ya Boston na hata matokeo ya mechi mbili za fainali za AFCON, ambapo moja mshindi alikuwa Zambia na nyingine Nigeria ilichukua ushindi. Amesha wahi kutabiri kuhusu kifo cha Rais mmoja wa Afrika na inasemekana Bingu Mutharika wa Malawi ndie aliyetabiriwa wakati huo. Pia anasemekana kutabiri kuhusu ndege ya Malaysian Airline iliyopotea baharini, miezi kadhaa kabla ya tukio hilo.

No comments:

Post a Comment