Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, December 28, 2015

WATOTO WA WAHADHIRI WA UDSM WAJUMUIKA PAMOJA KWENYE 'GET TOGETHER' YA NGUVU

Watoto wa Chuo waliowahi kuishi chuoni hapo wakiwa kwenye picha ya pamoja hakika hii ilikuwa ni party ya nguvu. Watoto wa chuo waliokuwa wakiishi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakati wazazi wao wakiwa ni wahadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Ili kuweka ukaribu watoto hao wamekutana na kufanya party ya nguvu hivi karibuni katika viwanja vya UDSM hii ikiwa ni kurudisha ukaribu pamoja na kufahamiana kwa wale waliopotezana miaka kadhaa chuoni hapo.
Hakika ilikuwa ni siku ya furaha maana watu walikuwa wanakumbushana mambo ya miaka ya 90 kwani kipindi hicho walikuwa wadogo.
Watoto wakiendelea kucheza wakati wa party ya watoto walioishi chuoni hapo kipindi wazazi wao bado ni waalimu katika chuo cha UDSM

 
Full Happy kwa kila tu aliyefika katika Party hiyo.
Watoto wa wahadhiri wa UDSM wakibadilishana mawazo kwenye party ya kuwaunganisha pamoja kama wanafamilia wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Hakika watoto walikuwa waki-enjoy vya kutosha maana hakuna aliyeboreka kwani kulikuwa na kila aina ya michezo kwa watoto wa rika zote.

Baadhi ya watoto wakiwa wametokelezea kwenye ukodak.

Baadhi ya watoto walioishi Chuoni UDSM wakiangalia vitabu pamoja na kununua vitabu hii ikiwa ni kundeleza utamaduni wa kujisomea.
Hakika ilikuwa shangwe kwa watoto walioishi chuoni hapo wakati wazazi wao ni wahadhiri chuoni hapo
Hivi ni Baadhi ya vitabu vilivyokuwa vinauzwa wakati wa Party hiyo iliyofanyika chuoni hapo.
Muda wa kuserebuka ulifika sasa kila mtu akaanza kuonesha umahiri wake kwenye kulisakata Rhumba.
Watoto wa Chuo wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kumaliza party yao.

No comments:

Post a Comment