Sehemu ya wanafunzi Shule ya watoto wenye ulemavu wa ngozi Buhangija iliyoko mkoani Shinyanga
Mbunge wa Kigoma mjini Mhe. Zitto Kabwe akiwa meza kuu na mrembo wa Tanzania Mwaka 2012, Brigitte Alfred
Baadhi ya anafunzi Shule ya watoto wenye ulemavu wa ngozi Buhangija iliyoko mkoani Shinyanga wakiwaimbia wageni wakati wa hafla hiyo
Mbunge
wa Kigoma mjini Mhe. Zitto Kabwe amekabidhi bweni la wanafunzi Shule ya
watoto wenye ulemavu wa ngozi Buhangija iliyoko mkoani Shinyanga baada
ya kutoa msaada wa kujenga bweni hilo.
Katika
makabidhiano hayo Mhe. Zitto alisema Tarehe 18 April mwaka huu
alitembelea Shule hiyo akiwa na Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo
Mama Anna E Mghwira kwa lengo la kusalimia watoto na walimu wao na
kutazama mazingira ya watoto.
"Nilifika
hapa kwa lengo la kuona mazingira ya shule na watoto niliona namna
Shule ambavyo inakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo haswa nafasi
za kulala, Nilishuhudia watoto wakilala karibu watano katika kitanda
kimoja. Niliumizwa sana," alisema Zitto kwa masikitiko.
Anasema alionyeshwa ujenzi wa Bweni jipya la watoto na kuelezwa kuwa
linajengwa na aliyekuwa mrembo wa Tanzania Mwaka 2012, Brigitte Alfred
kupitia Taasisi yake ya Brigitte Alfred Foundation.
Aidha
aliambiwa kuwa ujenzi umesimama kutokana na changamoto mbali mbali
ikiwemo ufinyu wa bajeti, "Wakati huo nilikuwa nimeng'atuka Ubunge na
nilikuwa nasubiri malipo ya kiinua mgongo Kwa mujibu wa Sheria, niliamua
hapo hapo kwamba sehemu ya gratuity yangu nitaitoa kama mchango wangu
katika juhudi za Briggitte kuboresha mazingira ya malezi ya watoto wetu
katika shule hii."
Zitto
alisema aliamua pia kusaidia matibabu ya saratani watu wenye ulemavu
wa ngozi katika hospitali ya Ocean Road, Dar Es Salaam kupitia fedha
hiyo.
NaAlisema anamshukuru Mungu kwamba alimuwezesha kutimiza dhamira yake
hiyo na hivyo kuchangia juhudi hizi za Briggitte Alfred Foundation kwa
Gratuity yake yote ambao sasa umekamilika.
"Leo
tupo hapa Buhangija kushuhudia ukamilifu wa kazi hii adhimu, nampongeza
sana Miss Tanzania 2012 kwa mradi huu unaotoa changamoto kwa watanzania
wengine kutumia nafasi zao katika jamii kusaidia jamii yetu," alisema
Zitto.
Zitto
aliitaka Serikali kuhakikisha kuwa Shule muhimu kama Buhangija zinapata
uangalizi maalumu kwani mahitaji yake ni maalumu.
Alisema nchi yetu haiwezi kuwa na sifa yeyote nzuri duniani kama bado
kuna baadhi ya raia wake wanaishi kwa mashaka na hofu ya maisha yao
hivyo ni wajibu wa viongozi kuhakikisha kila mtanzania anajivunia badala
ya kuvumilia Utanzania wake.
Wageni na sehemu ya wanafunzi Shule ya watoto wenye ulemavu wa ngozi Buhangija iliyoko mkoani Shinyanga
No comments:
Post a Comment