Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, January 8, 2016

KOCHA ROGASIAN KAIJAGE AJIUZULU TWIGA STARS.


KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Mpira wa Miguu (Twiga Stars), Rogasian Kaijage amejiuzulu nafasi hiyo kuanzia jana baada ya kuomba kwa uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF).
Kaijage aliiongoza Twiga Stars kwenye fainali za michezo ya Afrika (All Africa Games) zilizofanyika nchini Congo Brazzavile Septemba mwaka jana, baada ya kuiondoa timu ya taifa ya Zambia katika hatua ya mtoano.
TFF imesikitishwa na taarifa za kujiuzulu kwa kocha huyo mwenye leseini A ya CAF, ambaye amekuwa akizinoa timu za taifa za wanawake ya wakubwa (Twiga Stars) pamoja na timu ya wanawake wenye umri chini ya miaka ya 20 (Tanzanite) tangu mwaka 2013.
Kufuatia kujiuzulu kwa kocha Kaijage, TFF inaendelea na programu za maendeleo ya soka kwa wanawake, ikiwemo kuendesha ligi ya wanawake (Tanzania Women League).
TFF inamtakia kila la kheri kocha Rogasian Kiajage katika shughuli zake.

 
Aidha maandalizi ya mchezo kati ya Twiga Stars dhidi ya Zimbambwe yataendelea chini ya kocha atakayeteuliwa kuchukua nafasi yake, mchezo utakaochezwa mwezi Machi mwaka huu na mshindi kucheza na Zambia.
TFF itaendelea kupambania kwenye maendeleo ya soka la wanawake.

No comments:

Post a Comment