Moja ya Suzuki Grand Vitara magari ya CFAO yaliyopo kwenye maonyesho ya bidhaa mpya walizonazo katika jengo la PSPF Golden Jubilee Tower lililopo Posta jijini Dar es Salaam.
Gari hilo la Suzuki Vitara linavyoonekana kwa nyuma.
Gari hilo aina ya Suzuki Grand Vitara linavyoonekana ubavuni.
Moja ya Suzuki magari ya CFAO yaliyopo kwenye maonyesho ya bidhaa mpya walizonazo katika jengo la PSPF Golden Jubilee Tower lililopo Posta jijini Dar es Salaam.
Gari hilo la aina ya Suzuki linavyoonekana ubavuni..
Suzuki hiyo inavyookena upande wa nyuma.
Gari ndogo Suzuki OMNI inavyookena kwa mbele.
upande wa ndani unaogawa gari hilo la Suzuki ambao unaonesha upande wa dereva na upande ambao mtu anaweza kutumia kwa kuweka mizigo na mambo mengine.
upande wa nyuma wa ndaniu wa gari hilo aina Suzuki OMNI.
Magari hayo yanavyoonekana katika showroom hiyo ndani ya jengo la PSPF Golden Jubilee Towers.
Kampuni
ya uuzaji magari ya CFAO imefanya onyesho la kuonyesha bidhaa mpya
walizonazo katika jengo la PSPF Golden Jubilee Tower lililopo Posta
jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
na Modewji Blog, Meneja Masoko wa CFAO Motors, Sheikha Said amesema
sababu ya kampuni hiyo kufanya onyesho katika jengo hilo ni kuwaonyesha
wateja wa kampuni hiyo bidhaa mpya walizonazo katika sehemu zao
wanazouzia magari (showroom).
Amebainisha
kuwa, mbali na kuwaonyesha wateja lakini pia kuwaonyesha wafanyakazi na
wananchi mbalimbali ambao walikuwa hawajui bidhaa zinazopatikana CFAO
Motors au kwa wengine kuwa na shughuli nyingi hivyo kushindwa kufika
katika 'showroom' zao na kupitia onyesho hilo wataweza kupata magari
katika maeneo yao ya kazi.
“Tupo
hapa kwa hili kuwasogezea huduma watu wa aina mbalimbali na wafanyakazi
wa taasisi mbalimbali waone bidhaa tulizonazo,” alisema Bi. Said.
Nae
Afisa Mauzo wa Suzuki, David Kritsos alisema kupitia onyesho hilo
wananchi na wafanyakazi wa ofisi mbalimbali wanaweza kununua magari
wanayopendelea na wanaweza kusaidiwa na CFAO Motors kupata mkopo benki
ili waweze kupata fedha za kununua magari hayo na kulipa mkopo taratibu.
Alisema
CFAO ndiyo kampuni pekee nchini yenye nafasi ya kusambaza bidhaa za
Suzuki na magari yote wanayoyauza bado ni mapya yakiwa bado hayajatumika
kabisa.
Showroom hiyo itaendelea hadi hapo 4 Februari.
No comments:
Post a Comment