Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, February 29, 2016

IBRAHIM AJIB AKABIDHIWA TUNZO YA MCHEZAJI BORA

Katika kuongeza morali na kuwazawadia wachezaji wanaofanya vizuri, Klabu ya Simba ilianzisha Tunzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi kuanzia mwezi wa Septemba 2015.
Mshindi wa mwezi wa Disemba, 2015 ni Ibrahim Ajib ambapo amepata kura nyingi zaidi zilizopigwa na mashabiki na wapenzi wa Simba na soka wa Tanzania kwa ujumla kupitia simu za mkononi ambao pia wamejiunga na huduma ya Simba News.Akikabidhiwa tunzo pamoja na pesa taslim Tsh 500,000/= na Mkuu wa kitengo cha biashara na mipango kutoka EAG Group ambao ni washauri na watekelezaji wa Masoko na Biashara wa Simba, Richard Mvula, Ibrahim Ajib alisema “kila siku nimekuwa nikiendelea kujitahidi kufanya vizuri zaidi ili nami ifike siku niweze kukabidhiwa tunzo hii, kwakweli ni heshima kubwa sana kwangu, napenda kuchukua fursa hii kuupongeza uongozi mzima wa Simba kwa kuanzisha utaratibu huu, pia napenda 

 
kuwashukuru mahsbiki wangu ambao wamenipigia kura, wachezaji wenzangu kwenye kikosi cha Simba ambao kila siku tumekuwa tukishirikiana katika kazi yetu hii ya mpira, napenda kushukuru kwa sapoti kubwa ninayoipaa kutoka kwa familia yangu na mwisho napenda kumshukuru Allah kwa kuendelea kunibariki na neema zake kila siku”
Akimakabidhi tunzo hiyo Mkuu wa kitengo cha biashara na mipango kutoka EAG Group Richard Mvula alisema “kama mtakumbuka utaratibu huu ulianzishwa kwa ajili ya kuwapa motisha wachezaji wetu na sasa umekuwa ni utamaduni wetu katika kuwapongeza na kuonesha kuthamini jitihada zinazofanywa na wachezaji wetu katika kuutafuta ushindi wa msimu huu”
Napenda kuwakumbusha wanachama na wapenzi wa Simba kuendelea kuwapa sapoti wachezaji wetu kwani kwa sapoti yao ndio mafanikio ya timu yetu yanapopatikana, aliongeza Mkuu wa kitengo cha biashara na mipango kutoka EAG Group Richard Mvula
Akizungumza jinsi tunzo ya mchezaji bora itakavyoendeshwa, Mkurugenzi Mkuu wa EAG Group, Imani Kajula alisema “Wanachama na wapenzi wa Simba na wapenda michezo ndio watakao kuwa wanachagua mchezaji bora wa mwezi kwa kutuma jina la mchezaji wanayempendekeza kwenda kwenye namba 15460, Ni wale tu ambao wamejiunga na Simba News kupitia mtandao wa Voda na Tigo wataweza kupiga kura kuchagua mchezaji bora wa mwezi wa Simba”.
Tukumbuke kuwa unaweza kumchagua mchezaji bora wa mwezi ukiwa umejiunganisha na huduma ya Simba News kwa kutuma jina la mchezaji kwenda namba 15460. Zoezi la kumchagua mchezaji bora wa mwezi wa Januari, 2016 litaanza February 29 2016. Piga kura mara nyingi zaidi kuweza kumpata mchezaji wako bora wa Mwezi Januari, 2016.
Simba News ni huduma iliyoanzishwa na Simba ili kuwapa wapenzi wa Simba habari mbalimbali za Simba popote pale walipo ikiwemo matokeo, majina ya wachezaji wanaocheza mechi, usajili na habari nyingine za klabu ya Simba. Kujiunga na Simba News tuma neno Simba kwenda namba 15460 ni maalum kwa Tigo na Vodacom.

No comments:

Post a Comment