Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, February 2, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI AMHAMISHA NAIBU KATIBU MKUU KATIBA NA SHERIA KWENDA UTUMISHI NA UTAWALA BORA


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemhamisha Bi. Suzan Paul Mlawi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, kwenda kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Manejimenti ya utumishi wa umma na Utawala Bora.

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, imeeleza kuwa uhamisho huo umeanzia tarehe 26 Januari, 2016.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa pamoja na shughuli nyingine za Unaibu Katibu Mkuu, Bi. Suzan Paul Mlawi, atashughulikia eneo la Utawala Bora.
Nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria iliyoachwa wazi, haitajazwa kwa sasa.

Gerson Msigwa,
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU.
Dar es salaam.

01 Februari, 2016.

No comments:

Post a Comment