Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, February 29, 2016

WAZIRI MKUU MAJALIWA ATEMBELEA HOSPITALI YA MKOA WA MTWARA


 Wamawake wakiwa wametandika khanga kwenye wodi ya wazazi ya Hospitali ya Mkoa wa Mtwara, Februari 29, 2016.Waziri Mkuu, Kassim majaliwa alitembelea wodi hiyo na kukemea mtindo huo akiwataka wauguzi na waganga kutandika mashuka yahospitali ambayo alisema ana taarifa kuwa yapo ili kuepusha hatari ya wananwake hao kubeba magonjwa kupitia kahanga hizo watokapo hospitalini hapo.
 Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Waganga, Wauguzi na wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara wakati alipoitembelea Februari 29, 2016.

 
 Baadhi ya Wauguzi na Madaktari wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao hospitalini hapo Februari 29, 2016. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea msaada wa kujenga zahanati na nyumba ya mganga kwenye kijiji cha Nandagala, wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi. 

Msaada huo wenye thamani ya dola za Marekani 55,000 (sawa na sh. Milioni 119.35)   umetolewa na kampuni ya Huawei Technologies yenye makao yake jijini Dar es Salaam.  Pia wametoa kompyuta za mezani (desktop) 25 pamoja na UPS  25 kwa ajili ya shule tano za sekondari wilayani humo. 

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo jana (Jumapili, Februari 28, 2016) Mkurugenzi Mtendaji wa Huawei, Bw. Bruce Zhang alisema kampuni yake imetoa msaada huo ikiwa ni mwitikio wa sera ya Wizara ya Afya inayotaka kila kijiji kiwe na zahanati na kila kata iwe na kituo cha afya.

Wakati huohuo, kampuni ya mtandao wa simu ya Halotel ilimkabidhi  Waziri Mkuu hundi ya sh. Milioni 9/- ambazo ni mchango wao wa kumsaidia  Waziri Mkuu ambaye pia ni mbungewa jimbo la Ruangwa ili zisaidie kulipia familia zisizo na uwezo kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).

Akizungumza na wanakijiji hao kabla ya kukabidhi hundi hiyo, Meneja Mkuu Msaidizi wa Biashara wa Mkoa wa Lindi, Bw. Sebastian Innocent alisema: "Mchango huu utazihusu kaya 900 ambazo zinalipiwa sh. 10,000 kila moja. Kila kaya inatakiwa kulipia watu sita, hivyo tutaweza kuwafikia watu 5,400 kupitia mchango huu.

Alisema kampuni yao imejenga minara 50 katika mkoa wa Lindi ambapo 40 inafanya kazi na minara 22 kati ya 40 imeunganishwa na inatoa huduma ya 3G.  

Akitoa shukrani kwa misaada yote,  Waziri Mkuu alisema anaishukuru kampuni ya Halotel kwa kumsaidia kulipia sh. Milioni 9/- kwa ajili ya CHF ambazo alisema zimegawanywa katika vijiji 90 vya wilaya nzima ya Ruangwa na kwa kaya 10 za watu sita sita.

Aliwashukuru kwa kuweka minara katika wilaya hiyo jambo ambalo alisema litasaidia wananchi kupata mawasiliano ya simu kwa urahisi zaidi.

Kuhusu zahanati,  Waziri Mkuu Majaliwa aliishukuru kampuni ya Huawei Technologies kwa msaada huo ambao alisema utakapokamilika, utawapunguzia wananchi adha ya kwenda kijiji cha jirani kupata huduma ya matibabu. 

Alisema ana mpango wa kuweka nguvu ya umeme jua (solar power systems) kwenye shule zote za msingi, shule zote za sekondari  na zahanati zote kwenye wilaya ya Ruangwa ambayo ndiyo jimbo lake ili asiwepo mtoto wa kushindwa kusoma au mtu kupata matibabu kwa sababu ya kukosa umeme. Wilaya ya Ruangwa ina shule za msingi 82, shule za sekondari 15, vituo vya afya vitatu na zahanati 28.


Waziri Mkuu alirejea Mtwara jana hiyo hiyo na leo hii amerejea Jijini Dar es Salaam.
chanzo issa michuzi blog

No comments:

Post a Comment