Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, March 16, 2016

DHAMIRA YA MWIGULU YAANZA KUTIMIA, WAFUGAJI SASA KUPEWA BLOCKS WAFUGE KWA MFUMO WA KISASA


Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh. Mwigulu Nchemba akimuangalia mmoja wadume  la ng'ombe anayetumika kuzalisha Mitamba kwenye kitaru namba 9 shamba la kitengule-Karagwe.Baadhi ya ng'ombe waliopo kitaru namba 9 shamba la kitengule ambapo kwenye block hii moja kuna Ng'ombe zaidi ya 800 wanaolishwa na kuhudumiwa vizuri na mmiliki wa kitaru hiki

 
.Ng'ombe wakitoka kuogeshwa kwaajili ya kuua baadhi ya wadudu kama kupe wanaopendelea kukaa kwenye mwili wa ng'ombe.Hili ni moja ya josho la kisasa ndani ya kitaru namba 9.

Kufuatia ziara ya waziri mkuu, Mh. Kassim Majaliwa ndani ya mkoa wa Kagera akiwa ameambatana na waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya ndani, Ziara hiyo imekuja na maagizo kadhaa ikiwamo wamiliki wote wa vitaru kwenye ranchi za Taifa ambao hawajaziendeleza waziachie mara moja na maeneo hayo yagawiwe upya, Waziri Mkuu ameagiza pia kwa wamiliki wa vitaaru ambao sio watanzania wajisalimishe au waondoke kwenye vitaru hivyo kabla hatua kali hazijaanza kuchukuliwa.
Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh. Mwigulu Nchemba akiwa na timu yake ya wataalamu wameshaanza kupitia vitaru vyote "blocks" na wamiliki wake ikiwepo pia idadinya mifugo kwa kila block,Hii leo Mwigulu Ncheba amekutana na wamiliki wa vitaru kwenye shamba la Kitangile-Karagwe na kuagiza wamiliki wote ambao hawajaendeleza maeneo wanayoyamiliki yanachukuliwa na serikali kwaajili ya kuwapatia watanzania wenye uwezo wa kuziendesha.
Mwigulu Nchemba ameagiza pia wamiliki wa vitaru kuacha mchezo wa kukodisha na kuingiza mifugo kutoka kwa wafugaji haramu wa nchi jirani,kitendo hicho ni kosa na yeyote atakayebainika anakwenda jela na adhabu kali itafuta.
Mbali na vitaru hivyo, waziri Mkuu akishirikiana na waziri wa kilimo wameagiza ofisi ya mkuu wa mkoa wa kagera kuondoa wavamizi wote kwenye pori tengefu ya serikali kabla hatua zingine zinazofuata kuanza kutekelezwa.
Kupitia uwekezaji mzuri kwenye kitaru namba 9 cha shamba la Kitengule,Mwigulu Nchemba ametoa rai kwa wafugaji wote nchini kuanza kujipanga kufuga kwa mfumo wa vitaru ili kuachana na ufugaji holela unaopelekea migogoro mbalimbali na wakulima.
Picha/Maelezo na Festo Sanga Jr.

No comments:

Post a Comment