Club ya soka ya Chelsea imekemea kelele ambazo zimekua zikisikika kutoka kwa mashabiki wa club hiyo dhidi ya beki wa qpr
Anthony Ferdinand wakati wa mchezo kati ya
Chelsea na
GENK Jana.
Mashabiki waliosafiri kutoka England mpaka ubelgiji, walikua wakiimba nyimbo za kumkashifu
antorn Ferdinand ambae inasemekana alitolewa maneno ya kibaguzi na mchezaji wa Chelsea
John terry wiki iliyopita.
Msemaji wa Chelsea amesema kwamba hawajafurahishwa na kilichofanywa na mashabiki hao na kama club hawataki ziendelee.
kocha wa chelsea Andre Villa Boas.
hata hivyo Kocha wa Chelsea andre villa boas amejiweka pembeni, kwa
kusema hana chochote cha kusema kuhusiana na walichokua wanaimba
mashabiki wa Chelsea jana.
jana mashabiki wa Chelsea, walikua wanaimba kwa kusema
anton Ferdinand unajijua wewe ni nani.
Na ilionekana kama wanazidi kukitonesha kidonda, kwa sababu tusi zito alilotukanwa na john terry lilisema wewe ni…… wa afrika….
neno zito limefichwa kwenye desh, sasa jana mashabiki wa Chelsea ndio walikua wanaiwekea chumvi hiyo kauli.
No comments:
Post a Comment