Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, November 3, 2011

ZITTO KABWE ndani ya Opareshen ya saa nne.


mbunge wa kigoma kaskazini, Zitto Kabwe amefanyiwa opareshen ya KIPANDAUSO leo, opareshen ambayo imedumu kwa saa nne kwenye hospitali ya Apollo, Bangalore -India.

hali ya sasa ya mbunge huyo ni nzuri, na kwa mujibu wa maelezo ya kaka yake ambae wako pamoja, ni kwamba wanatarajiwa kuruhusiwa kutoka hospitali siku tatu zijazo.

Salum amesema bado wako hospitali, na kwamba sasa hivi mbunge huyo japokua hawezi kuzungumza sana, amesema kichwa kilichomsumbua sana toka wiki iliyopita, hakimuumi tena, na pia damu hazitoki.



hii ni moja ya muonekano wa ndani wa hospitali ya Apollo - Bangalore.

Zitto Kabwe alisafirishwa ijumaa iliyopita kwenda India baada ya kugundulika kwamba hakukuwa na uwezekano wa kutibiwa bongo.

kuumwa kwa Zitto kulifanya baadhi ya taarifa za kupotosha kuenezwa kwa kasi kwamba mbunge huyo amefariki dunia.

hata hivyo hali yake imebadilika sio kama wiki iliyopita, ambapo juzi kwa mara ya kwanza, alipata nafasi ya kuzungumza na mashabiki zake kupitia kurasa zake za fB na twitter, na kuamplfy kwamba anaendelea vizuri, hivyo wasiwe na hofu yoyote

No comments:

Post a Comment