Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, August 20, 2012

Hamad Rashid ataka Maalim Seif afungwe




MBUNGE  wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed na wenzake wameendelea kuwang’ang’ania wadhamini wa Chama cha Wananchi (Cuf),  wakiiomba Mahakama Kuu iwatie hatiani na kuwafunga kutokana na kitendo cha kufukuzwa kwao uanachama. 
Licha ya wadhamini hao, wengine ni wajumbe wa Baraza Taifa la Uongozi la chama hicho akiwamo Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad.  Januari 10, mwaka huu Rashid na wenzake 10 waliwasilisha mahakamani hapo maombi wakitaka iwaite wadhamani wa chama chama hicho, wajieleze sababu za  kutotiwa hatiani na kufungwa kwa kosa la kupuuza amri ya mahakama. 

Maombi hayo yalitokana na uamuzi wa Baraza la Taifa la Uongozi la chama hicho wa Januari 4, mwaka huu kuwafukuza uanachama wa chama hicho na kuwasimamisha wengine.  Pia, katika maombi hayo wanaomba mahakama ibatilishe uamuzi wa Baraza hilo wa kuwavua uanachama kwa madai kwamba walikiuka Katiba ya Cuf.
Wakati wa usikilizwaji wa maombi hayo, Hamad na wenzake katika hoja zao za maandishi walizoziwasilisha mahakamani kupitia kwa Wakili wao, Augustine Kusalika wanadai baraza hilo liliwafukuza uanachama wakati tayati likiwa na amri ya mahakama kuzuia kuwafukuza.
Amri hiyo ya mahakama ilitolewa na Jaji Agustine Shangwa Januari mwaka huu  kufuatia maombi waliyoyawasilisha Januari 3, chini ya hati ya dharura. Mwisho

No comments:

Post a Comment