Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, August 7, 2012

Mashambulizi makali yatokea Ivory Coast



Wanajeshi wa Ivory Coast waliouawa

Majambazi waliokuwa wamejihami wameshambulia kambi ya kijeshi mjini Abidjan, mji mkuu wa Ivory Coast na kuwaua takriban wanajeshi sita.
Wenyeji walielezea kusikia milio ya risasi usiku kucha katika mtaa wa Riviera. Idadi kubwa ya wanajeshi wakiwemo walinzi wa amani wa umoja wamataifa, wamepelekwa katika eneo hilo ingawa sasa maafisa wakuu wanasema kuwa hali imeweza kudhibitiwa.
Mji huo ulishuhudia mapambano makali, mwaka jana wakati wa mvutano wa kisiasa ambao ulitokea baada ya matokeo ya uchaguzi ambayo yalizua utata mkubwa.
Mnamo siku ya Jumapili, wapiganaji waliokuwa wamejihami walishambulia kizuizi cha jeshi barabarani katika eneo la Yopougon mashariki mwa Ivory Coast pamoja na kituo cha polisi na kuwaua wanajeshi watano katika kambi ndogo ya kijeshi mjini Abidjan.
Wapiganaji hao walivalia sare za kijeshi na kutumia silaha nzito nzito japo hawakuweza kutambuliwa.

No comments:

Post a Comment