Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, October 22, 2016

MCHUNGAJI WA KANISA LA EAGT MITO YA BARAKA JIJINI DAR ES SALAAM AHUDUMU KATIKA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA.

Mchungaji  Bruno Mwakibolwa kutoka Kanisa la EAGT Mito ya Baraka Temeke Jijini Dar es salaam, jumapili iliyopita Oktoba 16, 2016 alihudumu katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya la Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, baada ya kuwasili katika kanisa hilo akitokea nchini Kenya.

Ilikuwa Ibada iliyojaa neema ambapo Mchungaji Mwakibolwa aliwahimiza waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya kumtumia Mungu kwa moyo wa kweli na watabarikiwa maishani mwao.

Alisema ziko njia mbalimbali za kumtumikia Mungu ikiwemo kuhakikisha waumini wanajikita katika kumjengea Mungu Makanisa bora ili kuwezesha neno la Mungu kusonga mbele.
Na BMG
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye ibada katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza
 
Mama Mchungaji, Mercy Daniel Kulola, akiwa katika ibada hiyo
Kiongozi wa timu ya kusifu na kuabudu, EAGT Lumala Mpya akihudumu katika ibada hiyo
Waumini wa EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza wakiwa kwenye ibada hiyo
Waumini wa EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza wakiwa kwenye ibada hiyo
Hii pia ni miongoni mwa njia bora kumtumikia Mungu
Kutoka kushoto ni Mchungaji wa Kanisa la EAGT Mito ya Baraka Jijini Dar es salaam, Bruno Mwakibolwa, Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola pamoja na Mama Mchungaji, Mercy Daniel Kulola.
Mmoja wa waumini wa EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza akiwa kwenye ibada hiyo
Waumini wa EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza wakiwa kwenye ibada hiyo.

1 comment:

  1. Great blog with loads of information. Great Article, I appreciate your effort in putting up this. We will love to let you know that there are available Post UTME past questions and answers.

    ReplyDelete