Mtendaji Mkuu wa Tanroads Mhandisi Mhandisi Patrick Mfugale (kushoto) na Mtendaji Mkuu kutoka kampuni ya ujenzi ya China Railway 15 Bureau group Corporation (CR15G) Zhang Tonggang (kulia) wakiweka saini mkataba wa ujenzi wa daraja la Kilombero lenye urefu wa meta 384 na ujenzi wa barabara zake za miingilio za lami( kilometa 9.142).na jenzi wake utagharimu shilingi bilioni 53.2 .Hafla hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.na kushuhudiwa na Waziri wa Ujenzi, Dkt, John Magufuli (mwenye miwani) na kulia kwake na katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Herbert Mrango.Pichani kutoka kushoto ni Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Tanroads , Bibi Hawa Mmanga,Mbunge wa Mikumi- Abdul Salim Ameir na Mbunge kutoka Morogoro Kusini Innocent Kalgeris Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale (kushoto) pamoja na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Ujenzi ya China Railway 15 Bureau Group Corporation (CR15G) Bw, Zhang Tonggang (kulia) wakibadilishana hati baada ya kuweka saini kwaajili ya ujenzi wa darala la Kilombero mkoani Morogoro, Daraja hilo lenye urefu wa kilometa 384 litagharimu shilingi bilioni 53.2. .Ujenzi wa daraja hilo utaziunganisha Wilaya za Mahenge na Ulanga. pamoja na kuboresha Usafiri wa mikoa ya kusini na kuleta kichocheo cha ukuaji wa shughuli za kiuchumi. (Picha na Mwanakombo Jumaa-Maelezo)
MIAKA 18 BAADAYE: JK AKUTANA TENA NA CATHERINE, BINTI ALIYEFANYIWA UPASUAJI
WA MOYO AKIWA NA MIAKA MINNE
-
RAIS mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo Mei 29, 2026
amekutana tena na Bi. Catherine P. Conrad Minja, aliyefanyiwa upasuaji wa
moy...
21 hours ago

No comments:
Post a Comment