Kikosi cha Kilimanjaro Stars.Picha na Bongo Staz
Kikosi cha Zanzibar Heroes.
historia ya kupeperusha bendera moja ya Tanzania kwa kucheza fainali
ya Kombe la Chalenji, lakini hilo linawezekana iwapo tu zitashinda
mechi zao za nusu fainali leo hii kwenye Uwanja wa Namboole.
Stars itaikabili Uganda, wenyeji wa michuano hiyo katika nusu
fainali ya pili, huku Heroes ikipepetana na Kenya katika mchezo
mwingine wa hatua kama hiyo utakaoanza mapema.
Stars na Heroes mara ya mwisho zilikutana hatua ya makundi
Stars na Heroes mara ya mwisho zilikutana hatua ya makundi
nchini Malawi, na Bara kulala kwa bao 1-0 na hivyo kukosa
nafasi ya kusonga mbele wakati Zanzibar haikuwa na la kupoteza
kwenye mchezo huo.
Timu hizo pia zinaweza kukutana zenyewe katika hatua ya kuwania
nafasi ya tatu, iwapo zote zitapoteza mechi zao mbele ya Kenya
na Uganda inayopewa matumaini makubwa ya kutetea taji.
Hata hivyo, dhamira ya kila upande ni kushinda mechi hizo na
kucheza hatua ya fainali ili kutwaa taji pamoja na kitita cha pesa
kutoka kwa wadhamini wa michuano hiyo, kampuni ya kutengeneza
bia aina ya Tusker.
Mtazamo wa kiupinzani unatarajia kuonekana kwenye mechi
zote zinazozikutanisha timu kutoka nchi waanzilishi wa Jumuiya
ya Afrika Mashariki, huku mchezo kati ya Uganda na Tanzania
ukionekana kuwa kiini cha ushindani.
Stars yenye kujiamini na kujivunia kiwango kizuri kuwahi
kushuhudiwa usoni mwa mwashabiki wa soka miaka ya
karibuni, itakuwa na kazi ya kulipa kisasi cha mabao 3-1
walichopata kutoka Uganda kwenye michuano iliyotangulia jijini
Dar es Salaam.
Kocha wa Stars Kim Poulsen anatarajiwa kuwapanga viungo wake
Kocha wa Stars Kim Poulsen anatarajiwa kuwapanga viungo wake
mahiri
Mwinyi Kazimoto na Salum Abubakar ili kuzima mipango ya
Mwinyi Kazimoto na Salum Abubakar ili kuzima mipango ya
The Cranes, ambayo hakuna shaka itaratibiwa na Geofrey Kizito na
Hassani Waswa.
Ili kuwadhibiti washambuliaji matata wa Uganda chini ya Brian
Umony, Kim atampanga Kelvin Yondan kucheza beki ya kati a
kisaidiana na Shomari Kapombe na pembeni watakuwa Amir
Maftah na Erasto Nyoni.
Katika ushambuliaji, Kim ataendelea kuwatumia John
Bocco na Mrisho Ngassa wanaoongoza kwa pamoja orodha
ya wapachikaji mabao ili kuhakikisha nyavu za The Cranes
zinakuwa hatarini ingawa watasaidiwa kwa karibu na Amri
Kihemba pamoja na Frank Domayo.
Akizungumzia mchezo huo, Kim alisema kuwa kikosi chake
Akizungumzia mchezo huo, Kim alisema kuwa kikosi chake
kipo katika hali nzuri kimwili na kiakili kuweza kuikabili
The Cranes na kupata matokeo mazuri.
Kwa upande mwingi, Kocha wa Heroes alisema kuwa kikosi chake
kina morali ya hali ya juu kushinda mchezo dhidi ya Kenya.
Chanzo:Mwananchi.
No comments:
Post a Comment