Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, February 26, 2013

PADRI MKUU KANISA KATOLIKI ,UINGEREZA AJIUZULU



O'brien anasema atapinga vikali tuhuma dhidi yake
Mmoja wa mapadre waandamizi wa kanisa katoliki nchini Uingereza amejiuzulu wadhifa wake kufuatia shutma za kwamba alikwenda kinyume na matakwa ya kipadre mapema miaka ya themanini.
Kardinal Keith O'Brien ameachia madaraka kama kiongozi mkuu wa kanisa katoliki nchini Scotland na hatarajii kusafiri kwenda Vatican baadaye mwaka huu kumchagua Papa ajaye baada ya baba Mtakatifu Benedict wa 16 kijuzuru.
BBC imeelezwa kuwa kiongozi huyo,ameshutumiwa na mapadre watatu wa kanisa hilo na hatua hiyo ya kujiuzulu ni tukio kubwa katika mwenendo wa kanisa katoliki ikizingatiwa kuwa Kanisa hilo limekuwa kwenye shutma za ulaji rushwa na matatizo ya kiongozi kwa siku za hivi karibuni.
Inaarifiwa Padre O'Brien aliwauvinjia heshima makasisi mingo mitatu iliyopita.
Hata hivyo, mwishoni mwa wiki, alisema kuwa anapinga vikali madai hayo.
Duru zinasema kuwa hatua ya kujizulu kwa padre huyo kunaongeza shinikizo kwa makadinali wengine wanaokabiliwa na tuhuma za walivyoshughulikia kashfa za ngono

No comments:

Post a Comment