Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, February 1, 2013

SUMALEE AFIWA NA BABA YAKE,ASHINDWA KUFIKA KWENYE MSIBA SABABU YA MATATIZO YA PASSPORT UINGEREZA.


Sumalee akiwa Uingereza ambako alikwenda toka december 2012 akiwa na Barnaba.
Miezi 8 toka mama yake mzazi afariki dunia, msanii wa bongofleva Sumalee amepata pigo jingine baada ya baba yake mzazi kufariki january 31 2013.
Taarifa zilizoifikia dj-sek.blogspot.com ni kwamba baba yake alifariki jana jioni wakati bado Sumalee yuko Uingereza kwa shughuli za kimuziki.

Namkariri akisema “mama yangu amekufa kwenye mikono yangu, yuko kwenye mapaja yangu na mikononi nilikua namsomea dua tu”
Kulikua kuna taarifa kwamba Sumalee kapata matatizo ya hati yake ya kusafiria huko Uingereza hivyo itakua ngumu kuja Tanzania msibani lakini taarifa nilizonazo kutoka kwa mtu wa karibu ni kwamba hajapata tatizo lolote kama wengi wanavyodhani, kilichotokea ni kwamba alitaka kuongeza miezi sita ya kuendelea kukaa Uingereza hivyo ikabidi Passport aiache ubalozini ambapo ghafla ndio akapata msiba hivyo itabidi asafiri kwa kutumia documents.
Mtu huyu wa karibu wa Sumalee ameiambia  dj-sek.blogspot.com kwamba baba mzazi wa Sumalee anazikwa leo february 1 2013 na Sumalee wamejaribu kuwasiliana nae hapatikani kwenye simu hivyo hakuna uhakika kama yuko kwenye ndege kuja Tanzania ama la.
dj-sek.blogspot.com inatoa pole kwa Sumalee, familia na ndugu kwa msiba huu.

No comments:

Post a Comment