Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, March 27, 2013

Boscos Ntaganda: Sina hatia aiambia mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC



Congolese warlord Bosco Ntaganda looks on during his first appearance before judges at the International Criminal Court in the Hague, March 26, 2013.
Bosco Ntaganda akiwa kwenye mahakama ya ICC mara baada ya kufikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza




Kwa mara ya kwanza akipandishwa kizimbani kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ya ICC, jenerali Bosco Ntaganda amesisitiza kuwa hana hatia kuhusu tuhuma zinazomkabili mbele ya mahakama hiyo.
Akiwa amevalia suti nyeusi na akiwa amenyoa nywele zote, Bosco Ntaganda bila ya kung'ata maneno amewaambia majaji wanaosikiliza kesi yake kuwa hata hatia kwenye makosa ambayo yamewasilishwa mbele yake na ofisi ya mwendesha mashtaka.

Majaji wa mahakama hiyo wamepanga kuanza kusikiliza kesi za Ntaganda tarehe 23 ya mwezi September mwaka huu.

Bosco Ntaganda alijisalimisha Jumatatu ya wiki iliyopita kwenye ubalozi wa Marekani mjini Kigali Rwanda katika tukio ambalo liliishangaza dunia kwakuwa haikutarajiwa kwa kiongozi huyo kujisalimisha kwa hiari yale mwenyewe.

No comments:

Post a Comment