Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, March 11, 2013

Madereva wa wabunge walia njaa!



WAKATI wananchi wengi, wakikabiliwa na ugumu wa maisha, madereva wa wabunge nao wameibua kilio chao wakilalamikia ukali wa maisha. Madereva hao, walilazimika kumwandikia barua Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila wakilalamikia haki zao kukaliwa na wabunge. MTANZANIA imefanikiwa kunasa barua hiyo ya Julai, 2012 ambayo imesainiwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Madereva wa Wabunge, Juvenille Joseph. 

Pamoja na mambo mengine, barua hiyo inaishutumu Ofisi ya Bunge kushindwa kusimamia maslahi yao, hali inayowafanya waishi kwa shida.

Katika barua hiyo, madereva hao walilamikia suala la ukosefu wa mikataba ya kazi, huku wakitaka posho na mishahara yao itenganishwe kutoka katika akaunti za wabunge.

“Mheshimiwa Katibu wa Bunge, sisi ni madereva wa waheshimiwa wabunge, tunaleta kwako hoja zetu ili ziweze kupatiwa ufumbuzi wa kina katika ofisi yako.

“Kwa kipindi chote, madereva wa wabunge hatukuwa na mikataba ya ajira zaidi ya makubaliano ya mdomo baina ya dereva na mbunge.

“Ndiyo maana kunakuwa na unyanyasaji mkubwa kwa baadhi ya waheshimiwa wabunge dhidi ya madereva wao.

No comments:

Post a Comment