Msanii wa bongo fleva mwenye mafanikio makubwa zaidi Tanzania Diamond Platnumz, jana (June 19) amekutana na aliyekuwa rafiki wa karibu wa marehemu Albert Mangwea anayefahamika kama M 2 The P, na inavyoonekana wana mpango wa kufanya kitu pamoja.
Platnumz ameweka picha katika website yake akiwa na M 2 The P ambaye sasa anaonekana mwenye furaha inayoashiria kuimarika zaidi kwa afya yake.
Katika picha hizo Diamond aliandika,
“Siku ya jana katika mishe mishe zangu nilikutana
na ndugu yetu na mwanmuziki mwenzetu,M 2 the P ambae
alikuwa ni mtu wa kalibu na
marehemu Ngwair…kukutana kwetu tulipata fursa ya
kuzungumza mengi nna Mungu akipenda..maybe we gonn do
something”
Diamond-3
Hit maker huyo wa ‘Kesho’ yuko katika maandalizi ya mwisho ya safari yake ya Comoro anayotegemea kwenda kufanya show hivi karibuni.
Sheikh Mkuu wa Tanzania awahimiza Wanawake kumiliki Ardhi baada ya kupata
Hati Samia Ardhi Kliniki
-
*Dar es salaam – 05/03/2026*
*Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir, ametoa wito kwa
Watanzania kujitokeza kwa wingi kutumia fursa ya huduma z...
12 minutes ago


No comments:
Post a Comment