Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, June 9, 2013

TEMBO 39,000 WAUWAWA NA MAJANGILI



untitled2 3043c
Mratibu wa SPANEST, Godwell ole Maing'ataki
TEMBO 39,000 wameuawa katika kipindi cha mwaka 2009-2012 katika mapori ya Selous, Hifadhi ya Taifa Ruaha na Pori la  Akiba  la  Rungwe , Kizigo, Mapori ya Kigosi –Moyowosa  na Rukwa  katavi.
Hayo yalielezwa na Mratiba wa Mradi wa Kuboresha Mtandao wa Maeneo ya Hifadhi Kusini mwa Tanzania (SPANEST), Godwell  Meing’ataki  alipokuwa akiwakilisha mada katika kikao cha wadau wa ulinzi wa mali asili kilichofanyika kwenye ukumbi wa siasa ni kilimo Manispaa ya Iringa.
Alisema idadi ya Tembo imepungua kutoka 109,000 mwaka 2009 hadi 70,000 mwaka 2012  hivyo kupata idadi ya Tembo walio uwawa kuwa 39.000
Meing’ataki alisem utafiti unaonyesha kichocheo cha Ujangili ni biashara ya Meno ya Tembo inayo fanywa na wanunuzi toka China na Mataifa mengine ya Asia kwasababu ya urahisi wa kupata menoya Tembo.
Uwepo mpango wa kudumu kuongeza fedha za kusaidia kuwezesha kazi endelevu ya kupambana na ujangili,  Matumizi ya teknolojia ya mawasiliano
Urekebishaji wa sheria ikiwamo na kuanzisha ushirikiano wan a Mtandao wa wadau.

Kwa kuwa na mahusiano na nchi Mataifa yenye kuhifadhi Tembo kwa ajili ya kushirikiana katika jukumu la kudhibiti usafilishaji wanyamapori  ikiwa pamoja na ushawishi wa kisiasa na kidiplomasia ni muhimu kufanyika kampeni za mawasiliano katikanchi wanunuzi wa meno.
Alisema ili kufanikisha yote hayo yafaa kujenga mifumo ya mawasiliano
kuwezesha Askari wa doria kuwasiliana kwa urahisi katika mapori na vijijini piakuwepo na Mifumo ya uchunguzi na kubadilishana taarifa kwa kutumia teknolojia ya kisasa na kuhuisha mitandao ya kikale kwa Mfano mtoa habari, Kuwageuza majangili kuwa walinzi wakanufaika kihalali zaidi sawa na watakavyo tumika kwa uhifadhi wa Maliasili. Chanzo: mjengwablog

No comments:

Post a Comment