Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, July 18, 2013

MBEYA CITY YAANZA MAZOEZI MAKALI, MWAMBUSI AWEKA HADHARANI MATARAJIO YAKE LIGI KUU!!

Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Maandalizi ya kuelekea msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajiwa kuanza kushika kasi Agosti 24 mwaka huu yanazidi kushika kasi kwa timu shiriki kujifua vikali sana.
Huko jijini Mbeya, klabu mpya ya ligi kuu, Mbeya City, imeanza mazoezi makali ya “Gym” na kukimbia kwa kasi ili kutafuta pumzi ya kuhimili mitanange ya ligi kuu.
Kocha mkuu wa klabu hiyo, Juma Mwambusi amezungumza na FULLSHANGWE kwa njia ya simu kutokea jiji la kijani na kueleza kuwa kwa sasa ni ngumu kutathimini maendeleo ya kikosi chake kwani ndio kwanza wanaanza mazoezi, lakini kwa siku chache alizowaona vijana wake wameonesha morali na uwezo mzuri.
“Ndio kwanza nimeanza kujifua vijana wangu, baada ya wiki moja na nusu hivi, nitaeleza namna kikosi changu kinavyoendelea, pia nitaweka wazi program ya mechi za kirafiki, lakini kwa kifupi mechi za kujipima uwezo zitaanza kufanyika mwezi wa nane”.Alisema Mwambusi.
488123_216997305113321_161758080_n1Mwambusi aliongeza kuwa wanatambua wazi kuwa ligi kuu ni ngumu, lakini wanajiandaa vizuri kuhakikisha wanashindana na sio kushiriki.
Pia kocha huyo alisisitiza kuwa yeye ana uzoezfu mkubwa na ligi ya Tanzania, kwani aliwahi kuiongoza Tanzania Prisons kwa mafanikio makubwa, hivyo matarajio yake ni kupata mafanikio makubwa zaidi ya yale aliyowahi kupata akiwa na maafande wa jeshi la Magereza wa jijini Mbeya maarufu kwa jina la wajelajela.
“Mashabiki wawe na subira na uvumilivu, ndio kwanza timu yao inaandaliwa, lakini nawasihi sana watuunge mkono,  pale ligi itakapoanza waje kujenga utamaduni wa kuhudhuria mechi zote kuona matunda ya kikosi chao ambacho kwa sasa kinapiga jalamba la nguvu”.
Mbeya City ni miongoni mwa timu tatu zilizopata nafasi ya kucheza ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao, timu nyingine ni maafande wa Rhino Rangers wa mjini Tabora na Wauza Mitumba, Ashanti United ya jijini Dar es salaam.
Msimu uliopita klabu za Africa Lyon ya jijini Dar es salaam, Toto Africa ya Mwanza na Polisi Morogoro zilishuka daraja na kuzipisha timu tatu mpya.
LIGI DARAJA LA KWANZA MBEYA CITY NA BURKINA FC JAMHURI MORO PIX NO 2Hapa Mbeya City walikuwa wanapambana na klabu ya Burkinfaso fc wakati wakisaka tiketi ya kupanda ligi kuu soka Tanzania bara
Picha kutoka Maktaba

No comments:

Post a Comment