POLISI
wapatao sita Jumamosi iliyopita walivamia nyumbani kwa staa wa filamu
Bongo, Wema Sepetu maeneo ya Kijitonyama kwa lengo la kumkamata kufuatia
kesi iliyofunguliwa katika Kituo cha Polisi Kawe jijini Dar.
Awali taarifa
zilidai kuwa, tuhuma zinazomkabili staa huyo asiyekaukiwa na matukio ni
za kumtukana na kumpiga vibao Godluck Kuyumbu ambaye ni meneja wa
hoteli moja maarufu jijini Dar. NA GPL
Baada ya kesi hiyo yenye jalada KW/RB5988/2013 SHAMBULIO kufunguliwa
kituoni hapo Julai 6, mwaka huu mishale ya saa 5 asubuhi, maafande hao
wakiwemo wa kike wawili wakiwa wamevaa kiraia walifika mtaa anaoishi
staa huyo na kuufunga kabla ya kwenda kugonga katika geti la nyumba
yake.
Mara baada ya kugonga geti hilo, alitoka mwanaume aliyefahamika kwa
jina la Petman, alipoulizwa kuhusu Wema, alijiumauma huku kijasho
kikimtoka kabla ya kutoa jibu la kwamba hakuwepo.
Majibu hayo hayakuwaridhisha polisi hao ambapo walilazimika kuzuia
kila gari lililokuwa linatoka getini hapo wakiamini huenda Wema
angetolewa kiujanjaujanja.
Hata hivyo, hawakufanikiwa kumuona ndipo walipolazimika kumuita
mjumbe wa eneo hilo na kuomba ruhusa ya kuingia ndani kufanya upekuzi
lakini hawakumtia mikononi na taarifa zikawa mwanadada huyo yuko
Zanzibar.
No comments:
Post a Comment