Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, July 10, 2013

Sema Sina Pesa SIO HAtuna Pesa::Milionea akodi ‘private jet’ kwa shilingi milioni 162 kumsafirisha paka wake kutoka Urusi hadi Marekani

Paka mwenye jina Marsik wa Urusi amesafirishwa na ndege binafsi ya Paramount Business Jets (PBJ), kutoka Urusi hadi Marekani kwa gharama ya dola laki moja ambazo ni sawa na shilingi milioni 162 za Tanzania.
Akisafiri kutoka Urusi hadi Marekani, Marsik anadaiwa kupata huduma ya nguvu kabla hajapanda na ndani ya ndege hiyo.
Vyeti vyake vya afya vinavyoonesha chanjo alizopata alivipata saa 24 kabla ya safari kuanza.
Tajiri huyo anadai kutumia kiasi chote hicho ili kuhakikisha kuwa paka wake anafika Marekani salama na kuepuka kunyanyasika ama kifo kwakuwa baadhi ya wanyama wanaosafiri kwa ndege za kawaida huwekwa kwenye sehemu ya mizigo hupoteza maisha.
Source: prweb.com

No comments:

Post a Comment