Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, August 29, 2013

BASI LAPINDUKA, LAJERUHI 40 LIKIELEKEA TABORA


Basi la Bedui lenye namba za usajili T 273 ACX likirudishwa katika hali yake na winchi.
...Likiwa limelala baada ya ajali.
Basi la Bedui lenye namba za usajili T 273 ACX jana lilipinduka katika makutano ya barabara ya Tabora na ile iendayo Bukoba maeneo ya Nyihongo, Kahama mkoani Shinyanga. Watu 40 wamejeruhiwa katika ajali hiyo ambayo chanzo chake inadaiwa kuwa ni dereva kushindwa kukata kona iliyopo katika makutano hayo. Basi hilo lilikuwa likitoka Kahama kuelekea Tabora na kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kahama, hakuna abiria aliyepoteza maisha katika ajali hiyo, japo majeruhi sita walioumia sana wamepelekwa katika hospitali ya Bugando mkoani Mwanza kwa matibabu zaidi.
(Picha na Mdau Yohana Jackson)

No comments:

Post a Comment