Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, August 29, 2013

MHE. MBUNGE SAID AMOUR ARFI AFANYIWA UPASUAJI INDIA


IMG_4242

Na Walter Muguluchuma-mpanda
Mbunge wa Jimbo la Mpanda mjini ambae pia ni Makamu wa mwenyekiti wa Taifa wa chama  cha CHADEMA Said Amour Arfi amefanyiwa upasuaji wa nyonga Nchini India ambako alipelekwa kwa ajiri ya matibabu
Mdogo wa Mbunge huyo Nassor Arfi alisema kaka yake alifanyiwa upasuaji   hapo juzi katika hospitali ya Apolo ya nchini humo baada ya kupewa rufaa kutoka hospitali ya Taifa ya Muhimbili
Alisema   Arfi aliondoka hapa Nchini  Agosti 25  mwaka huu  majira ya saa tisa alasiri kwa  ndege ya  shirika la India akiwa amefuatana na mkewe ambapo walifika siku hiyo hiyo na kupitiliza kwenye hospital hiyo.

Alifafanua kuwa   mheshimiwa Arfi  afya yake ilianza kuteteleka toka  mwezi  wa juni mwaka huu .
Mwihoni mwa wiki alipo pewa rufaa ya kwenda kutibiwa Nchini India
Mdogo wake huyo alisema kuwa safari hiyo ya  kwenda kutibiwa Nchini India  imegharamiwa na ofisi ya Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania
Alisema hari ya mbunge huyo baada ya kufanyiwa upasuaji huo wa nyonga inaendelea vizuri na kwa sasa ameanza kuongea
Mwaka 2011  mbunge huyo aliwahi  kwenda  nchini India kwa matibabu kama hayo  mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa 2010

No comments:

Post a Comment