Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, September 7, 2013

FIESTA YAFUNIKA MKOANI MBEYA,TAZAMA PICHA NOMA SANAAAAA



Msanii wa muziki wa kizazi kipya,ambaye kwa sasa anafanya vyema kwenye anga za muziki huo,Neylee akiimba kwa hisi jukwaani huu wakati tamasha la Serengeti Fiesta likiendelea kwa shangwe ndani ya uwanja wa Sokonine.
Wakazi wa jiji la Mbeya wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013 ndani ya uwanja wa Sokoine,ndio kwanza shoo inaanza ambapo msanii aliyewahi kuiwakilisa shindano la BSS,Walter Chilambo ndiye aliyefungua pazia la onesho hilo usiku huu.
 Mama wa miduara ya Kibongofleva,Shilole akiwa na madensa wake wakitumbuiza jukwaani usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.
 Sehemu ya umati wa watu
 Wakazi wa jiji la Mbeya wakitoa heshima kwa baadhi ya wasanii waliotangulia mbele za haki, kwa kuwasha tochi za simu zao usiku huu.
 Rich Mavoko na skwadi lake wakilishambulia jukwaa. 
 Shilole akiimba jukwaani.
Wasanii mahiri katika miondoko ya hip hop,Stamina na Young Killer wakilishambulia jukwaa la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Sokoine usiku huu.
 Ni shangwe tu kwa wakazi wa jiji la Mbeya usiku huu ndani ya uwanja wa Sokoine. 
Mmoja wa sanii mahati wa kizazi kipya,Ommy Dimpo akiwaimbia mashabiki wake singo yake mpya iitwayo Tupogo usiku huu ndani ya tamasha la serengeti fiesta 2013.
 MKali wa kukamua mangoma kutoka Clouds FM,Dj Zero akiwarusha maelfu ya mashabiki wa muziki wa kizazi kipya wanaondelea kumiminika kwenye uwanja wa Sokoine usiku huu.
Msanii aliyewahi kulwakilisa shindano la BSS,Walter Chilambo ndiye aliyefungua pazia la onesho hilo usiku huu,pichani akitumbuiza mbele ya mashabiki wake.
Baadhi ya watu wakifuatilia yanayojiri usiku huu kwenye tamasha la Seremgeto Fiesta 2013 ndani ya uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.
Mkali wa Mahaba,a.k.a tajiri wa Mahapa kutoka mwambao wa Pwani,Cassi Mganga akiwaimbisha mashabiki wake usiku huu ndani ya tamasha la serengeti fiesta 2013,kwenye uwanja wa Sokoine mkoanni Mbeya.PICHA ZOTE NA MICHUZIJR BLOG

No comments:

Post a Comment