Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, September 5, 2013

KAULI YA PRUDYUZA SHEDY CLEVER KUHUSU WIMBO WA DIAMOND NA DAYNA NYANGE..!! AMALIZA UTATA KWA KUONGEA HAYA....


Ni baada ya sakata la kuibiana nyimbo lilichokua takribani siku mbili kati ya msanii Diamond Platnum na Dayna Nyange.
Na producer wa nyimbo hiyo akiwa na Shedy clever wa Burn recods.Team tizniz ikaamua kumtafuta Producer huyo ili kujua ukweli juu ya kitu hiki.
Shedy alisema “Beat hii nilitengeneza mimi kwa idea zangu mwenyewe,alivyokuja Dayna akaupenda ule mdundo,na mimi sikumnyima akafanya demo lakini hakulipia kabisa.Sasa ikapita zaidi ya miezi sita kila nikimuliza vipi anasema bado atakuja kufanya.Kuna siku Diamond akaja studio pale,akataka kusikia midumdo nikacheza midundo mbalimbali ila jamaa akavutiwa sana na ule mdundo ambao Dayna alifanya demo.
Mimi nikampigia Dayna na kumuelezea kwamba diamond kapenda kufanya kazi katika ile beat,Dayna akakubali kabisa,sasa nashangaa yeye kusema diamond kamuibia wakati alikubali kabisa.Mimi sina cha kusema zaidi ila ukweli upo hivyo.
Team tizniz

No comments:

Post a Comment