Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, September 19, 2013

MRISHO NGASSA AONYESHA JEURI YA FEDHA ANUNUA GARI LA MILLIONI 21 ATIMIZA MAGARI 10




Mkoko mpya wa Young Don; Gari jipya la Mrisho Khalfan Ngassa
ANA ‘wazimu’ wa magari. Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kuhusu ‘Young Don’ Mrisho Khalfan Ngassa, baada ya kutoa Sh. Milioni 21 kununua gari mpya aina ya Peugeot.


Ngassa katika gari lake jipya 


Sasa Ngassa anakuwa na gari 10, kati ya hizo kuna mbili alizowapa wazazi wake, baba na mama yake moja ya familia na tatu za kibiashara.



Kwa sasa, Ngassa ameuwambia mtandao wa BIN ZUBEIRY atakuwa anatumia zaidi ‘mkoko’ wake mpya badala ya ile Nissan ambayo amekuwa akionekana nayo siku za karibuni.
Wakati fulani, alionekana na Prado kwenye mazoezi ya Yanga na kuhusu gari hilo, Ngassa anasema; “Halikuwa gari langu lile, kuna mjomba wangu alichukua gari langu akaniachia lile la kwake,”alisema.  
Kwa sasa Ngassa yuko Mwanza alipokwenda kuhudhuria mazishi ya bibi yake mzaa baba, Bi Joha aliyefariki dunia mapema wiki hii.  
Magari ya Ngassa yamepagana nyumbani kwake

Ni gari kali


Mtoto huyo wa kiungo wa zamani wa Simba SC, Khalfan Ngassa ‘Babu’ anatarajiwa kupanda ndege leo mjini Mwanza kwenda Mbeya kuungana na timu yake, Yanga SC ambayo ipo huko kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya wenyeji Mbeya City kesho.
Hata hivyo, Ngassa kwa sasa hachezi kutokana na kuwa bado anatumikia adhabu ya kufungiwa mechi sita na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kusaini timu mbili, Simba na Yanga SC. Tayari amekosa mechi tatu.

No comments:

Post a Comment