Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, October 10, 2013

MABALOZI WA JUMUIYA YA NCHI ZA ULAYA (EU) WATEMBELEA GEREZA KUU UKONGA, JIJINI DAR ES SALAAM

image Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja akisalimiana na Balozi wa Jumuiya ya Ulaya Nchini Tanzania, Mhe. Gilberto Sebregondi ambaye aliongoza ujumbe wa Mabalozi wa Jumuiya ya Nchi za Ulaya katika ziara yao leo Oktoba 10, 2013 Gereza Kuu Ukonga, Jijini Dar es Salaam ili kujionea namna ambavyo Jeshi la Magereza linazingatia kikamilifu masuala ya Haki za Binadamu na Utawala Bora katika Uendeshaji wa Magereza hapa nchini.image (1) Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(kushoto) akisoma hotuba yake fupi mbele ya Balozi wa Jumuiya ya Nchi za Ulaya Nchini Tanzania, Mhe. Filiberto Sebregondi(aliyeketi mbele) pamoja na Mabalozi wa Jumuiya ya nchi za Ulaya wanaoonekana katika picha kabla ya kutembelea sehemu mbalimbali za Gereza Kuu Ukonga leo Jijini Dar es Salaam.
image (3) Mabalozi wa Jumuiya ya Nchi za Ulaya wakiwasilikiza kwa makini Wafungwa wa Gereza Kuu Ukonga, Jijini Dar es Salaam waliohukumiwa Adhabu ya Kunyongwa(hawapo pichani) ambapo wameiomba Jumuiya ya Ulaya kuendelea kupaza sauti na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili Adhabu hiyo hapa Nchini Tanzania iweze kuondelewa(wa pili kulia) ni Balozi wa Uingereza Nchini Tanzania, Mhe. Dianna Melrose.image (2) Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja( wa tatu kushoto mstari wa pili) akiongozana na Mabalozi mbalimbali wa Jumuiya ya Nchi za Ulaya kuelekea sehemu ya Zahanati ya ndani inayohudumia Wafungwa wa Gereza Kuu Ukonga, Jijini Dar es Salaam waliopotembelea leo Oktoba 10, 2013.image (4)Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wa Jumuiya ya Nchi za Ulaya mara baada ya kutembelea sehemu mbalimbali za Gereza Kuu Ukonga leo Jijini Dar es Salaam(wa tatu kushoto) ni Balozi wa Jumuiya ya Ulaya Nchini Tanzania, Mhe. Filiberto Sebregondi ambaye aliongoza Ujumbe wa Mabalozi hao(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment