
Brandts amemaliza mkataba wa kuitumikia timu hiyo katika mzunguko wa kwanza ambapo kwa sasa wapo kwenye mazungumzo na uongozi wa klabu hiyo kwa ajili ya kuingia mkataba mpya.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Bin Kleb alisema, wameshamalizana na kocha hivyo wanasubili akitua tu nchini Novemba 24 ndio wamsainishe mkataba mpya.
"Brandts anatarajia kutua nchini Novema 24 ambapo ndipo likizo yake itakuwa imefikia tamati kwa ajili ya kuja kukiandaa kikosi kwa ajili ya mzunguko wa pili.
"Mara tu atakapotua ndio tunaingianae mkataba mpya, hadi sasa hatujajua tutamsainisha wa muda gani lakini usiozidi chini ya mwaka mmoja," alisema Bin Kleb.

No comments:
Post a Comment