Damu salama ikiwa imehifadhiwa kwenye mfuko maalumu wa kutunzi damu. Picha na Maktaba
Dar es Salaam na mikoani. Wakati Serikali ikisisitiza kuwa huduma ya kumwongezea mgonjwa damu hospitalini ni bure, imebainika kwamba baadhi ya watu mitaani wakiwamo wabeba mizigo sokoni wanauza damu zao kwa watu wanaohitaji.
Mbali ya watu kuuza damu zao, majimaji hayo
mekundu muhimu mwilini yamegeuka bidhaa adimu baada ya baadhi ya wauguzi
na madaktari nao kugeuza huduma hiyo kuwa kitegauchumi chao.
Kwa mujibu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,
ni kosa kwa mtumishi yeyote wa afya nchini kumuuzia mgonjwa damu na wala
hakuna biashara ya kuuza damu kwa kuwa hutolewa bure na watu
wanachangia kwa hiari.
Uchunguzi wa kina uliofanywa na gazeti hili katika
hospitali mbalimbali nchini, umebaini hospitali nyingi hazina damu za
kutosha na hivyo kusababisha baadhi ya wagonjwa kuwalipa watu mitaani,
ili kuwatolea damu au kuinunua kwa wauguzi na madakari.
Hata hivyo, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa
Jamii, Dk Seif Rashid alisema kuwa wahudumu wa afya wanaoendesha vitendo
hivyo ni watu wanaojaribu kuizidi maarifa Serikali na kwamba wananchi
wamepewa taarifa za kutosha kuwa damu haiuzwi.
“Kuna watu wanajaribu kutuzidi maarifa, hiyo ni
tabia inayopaswa kupigwa vita. Mtu yeyote atakayetakiwa kununua damu,
atoe taarifa kwa mganga mkuu au kituo chochote cha polisi,” alisema.
Mkoani Dodoma
Wabeba mizigo wa soko la Majengo Mjini Dodoma,
wamekuwa mkombozi kwa wagonjwa wanaofika katika hospitali ya mkoa huo
baada ya kugeuza miili yao kuwa sehemu ya kuvuna damu na kuiuza kwa
ndugu wa wagonjwa hao.
Gharama za kuuza damu hiyo ni kati ya Sh10,000
hadi Sh30,000 kwa chupa moja, kutegemea na uwezo wa ndugu wa mgonjwa
huyo, lakini baadhi wamekuwa wakitoa zaidi kama sehemu ya shukurani.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na kuthibitishwa na baadhi ya
wabeba mizigo hao, imebainika kuwa kitendo cha kutoa damu kwa wabeba
mizigo ni cha kawaida na kwamba utaratibu huo ulianza muda mrefu.
Enock Ayub ambaye ni mmoja wa watu ambao
wamechangia damu zaidi ya mara tatu kwa nyakati tofauti, alilimbia
gazeti hili kuwa biashara ya kutoa damu anaipenda na kwamba inampa
matumaini ya kuishi kwa kuamini kuwa bado ni mzima.
“Mimi nimechangia damu zaidi ya mara tatu, lakini
tukifika kule tunabadilisha majina maana madaktari wanataka mtu ukae
muda za miezi sita bila ya kutoa, sisi tunataka fedha ‘mkwanja’, hatuna
jinsi,” alisema Ayubu na kuongeza:
Songea wanauza damu Sh 50,000
“Hata hivyo, napenda kutoa damu kwani ukiona wanakutoa ujue afya yako ni nzuri na huna Ukimwi na magonjwa mengine.”
Alipoelezwa hatari za kutoa damu mara kwa mara
bila kuzingatia ushauri wa daktari alisema, “Sioni tatizo maana fedha
tunazolipwa tunazitumia kunywa bia na matunda, hivyo afya zetu hurejea
kama kawaida, tena baada ya muda mfupi.”
Baadhi ya wodi ambazo gazeti hili lilitembelea na
kuzungumza na baadhi ya wagonjwa, lilibaini kuwa tatizo la damu katika
Hospitali ya Mkoa wa Dodoma limekuwa sugu, huku ndugu wa wagonjwa
wakilalamika kuwa wanauziwa damu kwa bei ya kati ya Sh40,000 hadi 60,000
kwa chupa moja.
“Mimi sitaki uniandike jina langu gazetini, lakini
ukweli ni kuwa madaktari walimpokea mgonjwa vizuri na damu aliwekewa
haraka sana tatizo likaja kwenye kuirudisha niliambiwa nitoe Sh60,000 au
mimi nitolewe damu, nilipogoma nikaonyeshwa Soko la Majengo kwa wabeba
mizigo,” anasema ndugu huyo.
Anasema kuwa alipofika kwa wabeba mizigo
walimuuliza daraja la damu aliyotoa na alipowatajia walijitokeza wawili
wenye daraja hilo wakaanza kupatana bei kabla ya kukubaliana na mmojawao
kwa kiasi cha Sh 25,000.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma,
Dk Nasoro Mzee, alikiri tatizo la damu ni kubwa katika hospitali hiyo na
kwamba linatokana na mwitikio mdogo wa wananchi katika kuchangia katika
benki ya damu.
Dk Mzee alisema hadi sasa kitengo hicho kina
upungufu wa damu na kwamba ni wanafunzi na askari tu ndio wanaochangia
damu kwa kiwango kikubwa.
“Wakifika watu ambao wana mahitaji ya haraka
tunachukua damu na kuwawekea, wengine ni kweli tunawaambia wachangiwe na
ndugu zao, na kwa wale waoga kutoa huwa wanakwenda kutafuta kwa
wanaojitolea kutoa damu,” alisema Mzee.
Alifafanua kuwa siyo kila damu inayotoka kwa mtu inakuwa salama kutumika, ni lazima ipimwe.
Songea wanauza damu Sh 50,000
Wabeba mizigo katika Manispaa ya Songea wamekuwa
wakichangia damu kwa wagonjwa wanaotakiwa kufanyiwa upasuaji au
kuongezewa damu, bei yao ni Sh50,000 kwa chupa ya ujazo wa lita moja.
Baadhi ya wauguzi pia wanadaiwa kujihusisha na biashara hiyo kwa bei ya
maelewano kati yao na mgonjwa au muuguzaji.
Akizungumza na gazeti hili mmoja wa wabeba mizigo
wa manispaa hiyo, Adrian Mbawala amesema biashara hiyo ameifanya kuanzia
mwaka 2006.
Mkoani Morogoro
Mkoa wa Arusha
Anasema wamekuwa wakipata wateja mbalimbali, wengi wakiwa ni
wajawazito pamoja na wanaotakiwa kufanyiwa upasuaji na waliopata ajali.
“Wanaotakiwa kufanyiwa upasuaji au waliopata ajali
tunawatoza kati ya Sh20,000 hadi 50,000 kwa lita moja, ila bei hiyo
inategemea na mahitaji ya mteja na uwezo wake kifedha” alisema.
Anasema licha ya kuwa biashara hiyo kuwa ya siri,
wao sio wanaotafuta wateja bali wateja ndio wanaowatafuta kwa lengo la
kutaka kuuziwa damu ili waweze kuwasaidia ndugu zao, “Ndugu wengi ni
waoga wa kutoa damu ndiyo maana wanatutafuta sisi.”
Mmoja wa wauguzi wa hospitali hiyo ya mkoa (jina
linahifadhiwa) amesema yeye binafisi hajawahi kufanya biashara hiyo ya
kuwauzia wagonjwa damu, ila amewahi kusikia baadhi ya wagonjwa
wakilalamikia kuuziwa damu na wauguzi na alipowahoji zaidi walidai
kuuziwa damu hiyo kwa Sh10,000kwa lita moja.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma, Dk
Benedicto Ngaiza amesema taarifa hizo siyo sahihi na hazina ukweli
wowote huku akisisitiza kuwa zinaenezwa na watu aliowaita wazushi.
“Hakuna mgonjwa anayeuziwa damu, wagonjwa
wanaohitaji kuongezewa damu huwa tunawaeleza ndugu zao kwa ajili ya
kuwachangia,” alisema Dk Ngaiza na kuongeza;
“Wanatakiwa kuchangia damu katika Kitengo cha Damu
Salama, cha kushangaza baadhi yao wanatafuta watu wa kuwapatia damu na
kuwalipa fedha. Wanapokuja nao hapa hospitali wanawatambulisha kama
ndugu zao, hivyo hospitali sidhani kama inahusika katika hili.”
Mkoani Morogoro
Mkazi mmoja wa Morogoro aliyejitambulisha kwa jina
moja la Msuya alisema kuwa baada ya kuelezwa na uongozi wa hospitali ya
mkoa huo kwamba ndugu yake anatakiwa kuongezewa damu chupa mbili,
aliishiwa nguvu na kujiuliza ataipata wapi damu.
“Ndugu yangu amelazwa wodi namba tisa, wamesema
ana upungufu wa damu, hospitali imesema itatoa chupa moja na sisi ndugu
tuchangie chupa moja, nilielezwa na mtu mmoja kuwa kama ndugu hawatakuwa
tayari wapo vijana wanaouza damu kwa Sh25,000 hadi 30,000” alisema
Msuya.
Mkoa wa Arusha
Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru,
imefanikiwa kupunguza tatizo la kuuzwa damu kwa wagonjwa kutokana na
kuwashirikisha wadau mbalimbali kutoa elimu ya kupinga biashara hiyo,
ikiwepo Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Jijini Dar es Salaam
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Dk Josia Mlay
akizungumza na gazeti hili alisema kwa sasa hospitali hiyo, licha ya
kupata damu asilimia 35 ya mahitaji kutoka benki ya damu, imeweka
matangazo katika wodi zote kuwa damu ni bure.
“Watu wengi hawapendi kutoa damu ila pale
wanapoombwa kusaidia wagonjwa wao wanaomba kuuziwa jambo ambalo ni
vigumu kulibaini na hata kama ukiwa na taarifa, waliouziwa hawasemi”
alisema Dk Mlay.
Dk Mlay alisema kama watu wakiwa na tabia ya
kujitolea damu ni wazi tatizo la damu kuuzwa litakwisha, kwani hata
wafanyakazi wengi wanajua wakibainika kuwa wanauza damu watachukuliwa
hatua.
Baadhi ya wagonjwa katika hospitali hiyo walisema,
“Ndugu hawatoi damu na hospitali wanasema hakuna damu ya kutosha sasa
unadhani utafanya nini, usipopata damu unakufa.”
Jijini Dar es Salaam
Jane Lyimo ni mkazi wa Jiji la Dar es Salaam na
siku za hivi karibuni alikuwa akimuuguza dada yake aliyekuwa amelazwa
katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke, “Dada yangu ana tatizo la
kupungukiwa damu, awali sikufahamu kama damu inauzwa hadi pale
nilipotakiwa kutoa fedha kwa ajili ya kulipia huduma hiyo.”
Anasema Septemba mwaka huu, dada yake aliwekewa
chupa mbili za damu lakini siku tatu baadaye wakati wakijiandaa kutoka
katika hospitali hiyo, muuguzi aliyekuwa akimhudumia dada yake alimtaka
kulipia Sh25,000 ili kununua damu nyingine, kufidia ile aliyowekewa dada
yake.
“Muuguzi alisema tunatakiwa kununua damu aina
yoyote (group lolote) ili ikawekwe kama akiba. Alitueleza kuwa kuna mtu
yupo katika hospitali hiyo kazi yake kubwa ni kujitolea damu na kama
tukitoa kiasi hicho cha fedha anaweza kutusaidia,” alifafanua.
Alisema baada ya kutoa Sh20,000 muuguzi huyo aliondoka na aliporejea aliwaeleza kuwa tayari damu hiyo imepatikana.
Katika Hospitali ya Mwananyamala Wilaya ya
Kinondoni mwandishi alikutana na Rachel Mhagama, kueleza kuwa amewahi
kununua damu mara kadhaa wakati akiwauguza ndugu zake.
Akisimulia zaidi Mhagama, alisema kwamba kaka
yake, ambaye kwa sasa ni marehemu alikuwa akihitaji kuongezewa damu, na
walipomweleza mhudumu alionekana kutokuwa na habari na mgonjwa wao,
kuongeza kuwa baadaye mtu mmoja aliwaeleza kuwa wanatakiwa kutoa fedha
ili mgonjwa wao aweze kuongezewa damu.
“Shemeji yangu alimwita muuguzi pembeni na
kumwingizia Sh13,000 mfukoni, tena ndiyo fedha pekee aliyokuwa amebakiwa
nayo. Baada ya hapo huduma zilianza kutolewa mbio mbio,” alisema.
Muuguzi atoa ushuhuda
Naye Hamida Yusufu, mkazi wa Mwananyamala, ambaye kwa muda mrefu
amekuwa akisumbuliwa na upungufu wa damu alisema kuwa siku moja
aliambiwa atoe fedha za kununulia damu baada ya kuelezwa kuwa damu
iliyokuwapo ilikuwa kundi tofauti na lake.
“Tuliambiwa tutoe fedha ili apatikane mtu mwenye
damu kundi moja na mimi. Ndugu zangu walitoa Sh10,000. Kitu ambacho
kilitushangaza, baada ya muda mfupi nililetewa damu na nikawekewa,”
alisema.
Katika hali isiyo ya kawaida mgonjwa mmoja katika
Hospitali ya Temeke, Hamida Hussein alisimulia namna mmoja wa wauguzi wa
hospitali hiyo alivyotaka kumwekea damu kundi tofauti na lake.
Alisema aliandikiwa chupa tatu za damu, kwamba
wakati wakati muuguzi akimwekea chupa ya pili, alikosea badala ya
kumwekea damu kundi O alimtundikia kundi B.
“Wakati alikuwa akijiandaa kunitundikia chupa ya
pili, nilishangaa kuona juu ya chupa hiyo imeandikwa ‘group B’,
nikamuuliza kwa nini wameamua kunibadilishia damu. Aliniangalia kisha
akasoma kwenye faili langu, halafu akaiondoa na kunitundikia nyingine,”
alisema.
Kwa mujibu wa Hamida, muuguzi huyo alimjibu: “Hata
kama usingeona ungeshtuka wakati damu inaingia mwilini, ungehisi hali
ya tofauti.”
Ofisa Uhusiano na Masoko wa Mpango wa Taifa wa
Damu Salama, Rajabu Mwenda alisema vitendo vya uuzaji damu vinavyofanywa
na wahudumu wa afya wasio waaminifu, vinarudisha nyuma jitihada za
taifa za kukusanya damu ya kutosha.
“Vitendo hivyo vinatuharibia taswira yetu, hebu
fikiria unamwomba mtu aje kujitolea damu bure halafu kesho ndugu yake
akiumwa anaambiwa anunue damu,” alisema.
Mwenda alisema watumishi hao wanatumia uhaba wa
damu uliopo nchini kufanya biashara na kuwataka wanaowafahamu
wanaoendesha vitendo hivyo kuwataja ili wakamatwe na kufikishwa
mahakamani.
Mpango wa Taifa wa Damu Salama kwa mwaka unakusanya asimilia 34 pekee ya damu inaohitajika nchi nzima.
Muuguzi atoa ushuhuda
Muuguzi mmoja ambaye jina lake linahifadhiwa kwa
sababu za kiusalama, alilisimulia Mwananchi Jumapili namna wahudumu wa
afya kwenye hospitali wanavyowauzia damu wagonjwa.
MAT wazungumza
Muuguzi huyo, ambaye kwa sasa anafanya kazi katika zahanati moja
wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam, alisema kuwa ili kupata damu
kwa urahisi kutoka kwenye benki za damu hospitalini ni pamoja na kusema
kuna mgonjwa ameokotwa na wasamaria wema na anahitaji damu haraka.
“Tulikuwa tukipewa ile damu tunawauzia watu wenye
fedha wanaotaka wagonjwa wao wahudumiwe haraka,” alibainisha na kuongeza
kuwa ingawa kila mhudumu wa afya anajua kufanya hivyo ni kosa. Hiyo
ilikuwa njia ya kupata fedha za ziada nje ya mshahara kirahisi.
MAT wazungumza
Kwa upande wake, Rais wa Chama cha Madaktari
Tanzania (MAT), Dk Primus Saidia alisema kuwa biashara ya kuuza damu
inachochewa na tabia ya baadhi ya watu wanaoogopa kupima damu ili
wawaongezee damu ndugu zao, ambao badala yake hutumia fedha kuwashawishi
madaktari na wauguzi wawauzie damu hiyo.
“Inafahamika kuwa benki ya damu ya taifa haina
damu ya kutosha, lakini pamoja na hivyo watu wanaotakiwa kupima ili
wawatolee damu ndugu zao wanaogopa. Badala yake wanatumia fedha
kuwahonga madaktari ili waipate kwa njia nyingine,” alisema.
MWANANCHI
MWANANCHI
No comments:
Post a Comment