Na Waandishi WetuSAKATA la kijana aliyejulikana kwa jina la Gabriel Nassana, mkazi wa Ghana jijini Mwanza kuua, kujeruhi kisha na yeye kujiua limeingia katika hatua nyingine kufuatia kuibuka madai kwamba, kamanda wa polisi wa mkoa mmoja nchini (RPC) ndiye chanzo.
Mchumba wa marehemu.Mauaji hayo yalitokea juzi nje ya nyumba ya wanafamilia waliokumbwa na dhahama hiyo iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Amani
kwa njia ya simu rafiki mmoja wa marehemu Gabriel (jina lipo) alisema
marehemu ambaye alikuwa mfanyabiashara wa magari jijini Mwanza aliaga
kwenda Dar kumchunguza mchumba wake (Christina) kwa sababu alidokezwa
kuwa shemeji yao huyo anamsaliti kwa kutembea na RPC ambaye jina lake
halikupatikana.
Alidai
kuwa, baada ya kufika Dar marehemu alimpigia simu na kumwambia kuwa,
habari za Christina kutembea na RPC huyo ni za kweli na kwamba amepata
habari anataka kusafiri hivyo hatakubali aende hiyo safari bila
kumfanyia kitu kibaya.CHANZO GPL

No comments:
Post a Comment