Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, November 26, 2013

Roma Asema Kuna Mashabiki Wake Hawajaona Video Ya 2030

Rapper ROMA Amefunguka leo kupitia sammisago.com kuwa bado vituo vya television Tanzania havijaitendea haki videoyake mpya ya 2030 ndio maana kuna mashabiki wake hawajaiona mpaka leo.
Kama kawaida kazi za Roma hupata wakati mgumu kupenyeza kwenye radio na tv kwa sababu ya ujumbe wa nyimbo hizo. Sababu hio imefanya kazi za Roma za Video kutazamwa zaidi kwenye mitandao kuliko kwenye television hapa Tanzania.

Video ya 2030 imetoka 11/11/2013 na imekuwa moja ya video iliyotazamwa sana youtube kwenye account ya Nisher ila bado 2030 haijapata muda wa kutosha hewani kupitia tv za bongo. Kuna mashabiki wa Roma waliopo sehemu za mbali na hawawezi kuiona kupitia youtube.chanzo SAMMISAGO

Mpaka leo video ya Roma ft Story - 2030 imetazamwa mara 21,574.



No comments:

Post a Comment