Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, January 21, 2014

AJALI YA BAJAJI YAUA MMOJA YAJERUHI WAWILI IRINGA USIKU WA KUAMKIA LEO

 Majeruhi  wa ajali ya  Bajaji Iringa  Karim Raphael (14) mkazi  wa Mshindo ' A' katika Manispaa ya  Iringa akiwa katika  Hospital ya  Rufaa ya  mkoa  wa  Iringa
 Majeruhi  wa ajali  ya Bajaji Idd Waziri Ng'eng'ena (17)  mkazi  wa  kijiweni mjini Iringa akiwa na majeraha  usoni  baada ya ajali  hiyo mbaya ya Bajaji iliyosababisha  kifo cha  dereva wa Bajaji  hiyo
 Muuguzi  katika Hospital ya  Rufaa ya  mkoa  wa Iringa  akimpatia matibabu majeruhi Karim
Idd na  Karim wakisubiri  kupelekwa wodini baada ya  kupatiwa matibabu ya  awali OPD 

AJALI mbaya  ya Bajaji yasababisha  kifo cha dereva  wake ambae ni mfanyakazi wa maduka ya Mzalendo mjini Iringa Bw Sudi Hashimu (22) mkazi  wa Mtwivila  huku wengine wawili  wakijeruhiwa  vibaya.


Ajali  hiyo mbaya  imetokea majira ya saa 2 usiku wa kuamkia  leo  katika  eneo la Mshindo mjini Iringa  wakati dereva  huyo wa Bajaji akijaribu  kukimbia baada ya  kudaiwa  kusababisha ajali katika  eneo la Miyomboni mjini Iringa.


Wakizungumza na mtandao wa www.matukiodaima.com majeruhi wa ajali  hiyo Karim Raphael na Idd Waziri Ng’eng’ena  walisema  kuwa kabla ya ajali  hiyo  dereva  huyo alikuwa amesababisha ajali kwa kumgonga mwendesha  Bajaji mwenzake na baada ya  tukio  hilo aliamua  kutimua  mbio kwa kutumia  usafiri wake wa Bajaji.


Kwani  walisema kufuatia ajali  hiyo eneo la Miyomboni ulizuka ugomvi kiasi cha aliyegongwa kupokonya  kofia (Helmenti) ya  Bajaji ya Sudi kabla ya marehemu  huyo  kufanikiwa kupokonya na  kukimbia .


“Katika Bajaji  marehemu alikuwa ametupakia abiria  watatu ambapo mmoja aliruka kabla ya  Bajaji hiyo kuchanganya  zaidi hivyo  tukabaki  abiri  wawili na dereva  mwenyewe …hata  hivyo alionekana  kuendesha  Bajaji  hiyo kwa  sifa zaidi na kuonyesha  kuwa  yeye ni bingwa wa  kukimbiza Bajaji  hiyo” alisema majeruhi Karimu


Hata   hivyo alisema baada ya  kufika  eneo la Mshindo Kanisani katika  tuta  kubwa dereva  huyo alishindwa  kupunguza mwendo na hivyo kulivaa tuta  hilo wakati akitaka kukata  kona na Bajaji  hiyo kuacha njia na kugonga ukuta wa uzio wa Kanisa la RC mshindo na dereva  huyo kutanguliza kichwa katika ukuta   huo huku  wao  wakifunikwa na Bajaji  hiyo.


Walisema kuwa  dereva  huyo alikufa  papo hapo huku wao  wakishuhudia  kifo chake kabla ya wasamaria  wema kufika na kuwaokoa.


Kwa  upande  wake  mmoja kati ya  shuhuda  wa  tukio  hilo Mood Mambo  alisema  kuwa alifika  eneo hilo na kukuta  wananchi  wakiendelea kutoa msaada  kwa  watoto hao ambao walikuwa  wamejeruhiwa  vibaya na mwili wa marehemu ukiwa  umepasuka  kichwa .

Majeruhi hao  walikimbizwa katika Hospital ya  rufaa ya mkoa  wa Iringa  huku mwili wa marehemu   huyu ukihifadhiwa katika chumba cha maiti katika Hospital  hiyo.
TUNAOMBA BOFYA HAPA NA ULIKE PAGE YETU KWA HABARI NYINGI MOTOMOTO(USIPITWEEEE)

Ajali  hiyo ni ya pili kusababisha kifo kwa mkoa wa Iringa na ajali ya tatu  mbaya  kutokea katika mkoa wa Iringa toka mwaka 2014 ulipoanza ambapo ajali ya kwanza  kusababisha kifo  ilitokea wilaya ya Mufindi nay a pili kujeruhi ilitokea eneo la Ilala wakati wa mkesha wa Mwaka mpya ikiwa ni dakika 20 kuukaribisha mwaka mpya na kupelekea dereva wa boda boda kukatwa mguu  wake nah ii ni ya tatu .

No comments:

Post a Comment