Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, January 30, 2014

CHAMA CHA WALEMAVU MANISPAA YA DODOMA CHITARA KIMEIOMBA HALMASHAURI YA MANISPAA YA DODOMA KUTEKELEZA AGIZO LA KUWAPATIA VIWANJA KWAAJILI YA KUJENGWA OFISI LILILOTOLEWA NA MKUU WA MKOA WA DODOMA.


PICHA NA MAKTABA
 
Akizungumza na dodoma  fm  Mwenyekiti  wa  walemavu bw. Hassan Sharrifu amesema wanaomba halmashauri kutekeleza  agizo la mkuu wa mkoa la  kuwapatia  viwanja  ili waweze kujenga ofisi itakayo wasaidia kuepukana  changamoto zinazo wakabili kutokana na kukosa ofisi.
Aidha bwana Sharrifu     amesema ni vema  manispaa   ikatambua shughuli zinazofanywa  na chama hicho ili iwape ushirikiano pale panapo hitajika kwani chama hicho kimekuwa kikijishughulisha na kazi mbalimbali          .
Nae mlemavu  wa  ngozi  bwana  Japheti  Andrea  amemuomba  Mkuu  wa Mkoa kuharakisha zoezi la kuwapatia walemavu maeneo ya kujenga ofisi hizo  ili waweze kuelezea  changamoto zinazowakabili katika chama hicho cha walemavu.
Hayo yamefuatia tamko lililotolewa na mkuu wa Mkoa wa Dodoma bi Rehema Nchimbi ambapo ameitaka manispaa iwapatie walemavu kutoka  kila wilaya eneo kwaajili ya kujenga ofisi.na DODOMA FM

No comments:

Post a Comment