Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, January 3, 2014

MASHINDANO YA MGIMWA CUP 2014 YAANZA KUTIMUA VUMBI JIMBO LA MUFINDI KASKAZINI


Mbunge  wa  jimbo la Mufindi kaskazin Bw Mahmoud Mgimwa akifungua mashindano  hayo
Mbunge  wa  jimbo la Mufindi kaskazin Bw Mahmoud Mgimwa akiwa na  wasomi  wa  vyuo  vikuu kutoka wilaya ya Mufindi 
 Mmoja kati ya  wana  vyuo  kutoka Mufindi  akizungumza na vijana .

TUNAOMBA BOFYA HAPA NA ULIKE PAGE YETU KWA HABARI NYINGI ZA KILA SIKU,(USIPITWEEEEEEEE)

 Mbunge  wa  jimbo la Mufindi kaskazin Bw Mahmoud Mgimwa akikabidhi  vifaa vya  michezo kwa  timu  shiriki 
 






 Mbunge  wa  jimbo la Mufindi kaskazin Bw Mahmoud Mgimwa akionyesha  uwezo  wake  katika soka kabla ya  kuzindua mashindano hayo


 JUMLA  ya   timu  5  za  jimbo la  Mufindi Kaskazin  zajitosa  kuwania  kombe la  Mbunge Mahmoud Mgimwa ( Mgimwa  Cup) katika  tarafa  ya Sadani .
 Timu   hizo  ni  kutoka  kijiji  cha  Ikweha,Ugenza,Ilangamoto, Sinai na Ukeremi ambazo   zote  zimepata  kutambaana  kuondoka na  ubingwa  katika  mashindano  hayo.
 Akifungua  pazia  la mashindano  haya  wakati  wa  hafla ya  kuukaribisha  mwaka mpya  2014  jana  katika  uwanja  wa kijiji cha Ugenza kata ya  Ikweha, Mgimwa  alisema  kuwa  lengo la mashindano hayo ni kuhamasisha  kasi  ya maendeleo kwa  vijana  kupitia  michezo .
Alisema  kuwa mashindano hayo yameanzishwa na kusimamiwa na shirika la Mgimwa foundation pamoja na umoja wawanafunzi walio maliza vyuo vikuu wilayani katika  wilaya ya Mufindi  (MUYOWIRUDE)
Mgimwa alisema nidhamira yake na viongozi anaoshirikiana nao kuhakikisha vijana katika jimbo lake wananufaika kwa kupitia michezo kasi  ya  maendeleo kwa  jimbo hilo kupitia  vijana  inazidi  kukua  zaidi
Mbunge   huyo  alisema zawadi mshindi wa kwanza atapata jumla ya Track suti 16 zenye thamani ya shiringi 480,000/=pamoja na mipira miwili yenye thamani ya shilingi 150,000 na  kufanya  zawadi  zote  kuwa na  jumla  ya Tshs. 630,000
 Huku mshindi  wa  pili atazawadiwa seti ya Jezi yenye thamani ya shilingi 250,000/=pamoja na mipira miwili ya Shilingi 150,000 na  kufanya zawadi zote kufikisha  kiasi cha  Shilingi 400,000 wakati mshindi wa tatu atapata mipira miwili yenye thamani ya shilingi 150,000
 Kabla ya  mashindano  hayo mbunge  huyo alikabidhi  seti ya Jezi  kwa  kila timu pamo na mpira mmoja wa mazoezi.
Pia alikabidhi mipira miwili kwa waamuzi wa mashindanohayo kwa ajili ya kushindania sambamba na hilo pia Mgimwa alisema atatoa zawadi mbali mbali kama .
  Kwa mfungaji wa goli la kwanza katika mashindano hayo atapata shilingi 20,000 mchezaji mwenye nidhamu atapata shilingi 30,000 na  timu yenye nidhamu itapata shilingi 50,000 huku mchezaji bora atapata shilingi 50,000
Hivyo  aliwataka  vijana kwa kupitia mashindano hayo kuhakikisha wana  wasikiliza vema  watakapo kuwa wakipatiwa mafunzo ya stadi za maisha kwakupitia wawezeshaji toka shirika la (MUYOWIRUDE).
Ambao wataenda sambamba na michezo hiyo kwani watapa kujifunza bure elimu  mbali  mbali .
Kiongozi wa  wanafunzi hao Marko Shayo alisema wao watatoa elimu yanamna yakujikinga na maambukizi ya Ukimwi,Elimu ya Ujasiriamali kwa kutumia zilizopo  katika jimbo  lao.CHANZO FRANSIS GODWIN

No comments:

Post a Comment