Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, January 16, 2014

MUDA WAONGEZWA KWA WAANDISHI WA HABARI KUWASILISHA KAZI ZAO KWAAJILI YA TUZO ZA AJAT 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwa niaba ya Kamati ya Maandalizi ya Tuzo za Umahiri za Uandishi wa Habari Tanzania(EJAT) 2013, imeongeza muda wa kuwasilisha kazi za kushindaniwa hadi Januari 21, 2014.Tarehe ya awali ya kuwasilisha kazi hiyo ilikuwa Januari 15, 2014.
 
Muda huo wa kuwasilisha kazi umeongezwa baada ya kuwepo kwa siku za mapumziko zilizofuatana na ofisi kufungwa, jambo lililowafanya baadhi ya waandishi washindwe kuwasilisha kazi zao kwa wakati. Vile vile hii ni fursa nyingine kwa waandishi wanaotaka kushiriki kwenye EJAT2013. Hata hivyo baada ya Januari 21, 2014  hakuna muda zaidi utakaoongezwa.
 
 Kamati ya Maandalizi ya EJAT 2013 inaundwa na Mfuko wa  Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), Johns Hopkins University, Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini Mwa Afrika –Tawi la Tanzania (MISA-Tan), Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira (JET), Jukwaa la Wahariri (TEF), HakiElimu, AMREF, ANSAF, BEST-AC, SIKIKA, Chama cha Waandishi wa Habari Dhidi ya Ukimwi ( AJAAT)  na Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT).

Kajubi D. Mukajanga 

Mwenyekiti Kamati ya Maandalizi ya EJAT 2013

No comments:

Post a Comment