Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, January 9, 2014

TANGAZO TOKA KWA MKURUGENZI WA MANISPAA YA KINONDONI KWENA KWA WAZAZI WOTE AMBAO WATOTO WAO WAMEFAULU LAKINI WAMEKOSA NAFASI.



Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni anawatangazia Wazazi wote wenye watoto waliofaulu mtihani wa Darasa la saba na kukosa nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza na ambao wako tayari kujiunga na Sekondari zenye nafasi nje ya Kata zao na Mji wa Kinondoni waende wakajaze fomu kwa Waratibu Elimu Kata.

Manispaa ya Kinondoni ina nafasi 2102 katika Sekondari za Goba, Fahari, Kibwegere, Kinzudi, Kwembe, Luguruni, Mabwe, Malamba Mawili, Mbopo, Mbweni na Njechele.

Mwisho wa kupokea maombi ni siku ya Ijumaa tarehe 10/01/2014.

wote mnakaribishwa.



ENG. MUSSA NATTY

MKURUGENZI WA MANISPAA

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI.

No comments:

Post a Comment