Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, February 1, 2014

Baba amuua mtoto kwa kumpiga na chupa ya bia kichwani

Alisema kuwa mumewe huyo wa ndoa alimuomba aende kumchajia simu barabarani ambapo alimuacha mdogo wake wa kike mwenye umri wa miaka 13 na mtoto akiwa anacheza kitandani.
Alisema mdogo wake alimwambia kuwa alimsukumiza kitandani akitaka kumbaka ndipo akapiga kelele na kufanikiwa kumchomoka na kukimbilia nje.
Matilda alisema kuwa baada ya kumwambia hivyo, yeye alianza kukusanya nguo za mdogo wake ampe ili aende nyumbani kwao ndipo mumewe huyo alipochukua kisu alichokiweka pembeni ya godoro na kutaka kumchoma nacho yeye.
Hata hivyo, Mungu mkubwa kwani Matilda alisema kuwa alifanikiwa kukidaka na kwa vile kilikuwa kibovu mwanaume alibaki na mpini yeye akabaki na kisu bila mpini.
Dakika chache baadaye mtoto alizimia hivyo baadhi ya majirani walimkimbiza katika Hospitali ya Boch iliyopo Kimara-Suka, Dar ambapo alipatiwa huduma ya kwanza kisha wakampiga X-Ray na kugundua kuna mshipa mkubwa wa fahamu kichwani ulikuwa umekatika.
Baada ya hapo alikimbizwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar. Alipofikishwa aliingizwa kwenye chumba cha upasuaji ili kuokoa maisha yake lakini ilishindikana kwani alifariki dunia.

No comments:

Post a Comment