Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, February 4, 2014

TATIZO LA USAFIRI KATIKA KIJIJI CHA SOLOWU WILAYANI CHAMWINO MKOANI DODOMA NI CHANZO KINACHOSABABISHA KUSHUKA KWA SHUGHULI ZA MAENDELEO KIJIJINI HAPO.


Wakizungumza na kituo hiki wakazi wa kijiji hicho  wamesema hali ya usari ni mbaya kutokana na  kutegemea gari moja kwa muda mrefu na kupelekea msongamano mkubwa wa watu .Aidha Bw Marino layachi  ameongezea kuwa  pamoja na  vyombo hivyo vya usafiri kuwepo ila bado havikidhi  mahitaji kutokukana na kuharibika mara  kwa mara.Nae afisa  mtendaji  wa kijiji hicho   Bw Yohana Mesai  amesema wame fikisha swala hilo sehemu husika lakini  hakuna  utekelezaji wowote ulifanyika  na  hivyo ameitaka   mamlaka  ya usafirishaji  majini na Nchi kavu (SUMATRA)  kuwajali wakazi wa vijijini .
kwa upande wake Afisa mfawidhi   wa mamlaka ya usafirishaji majini na Nchi kavu    kanda ya kati  Dodoma  Bw Bahati Musiba  amesema wao  wanatambua  safari zinazofanywa  kutoka Dodoma mjini  kuelekea Izava  hivyo amewataka   wamiliki   wa  vyombo  vya usafiri  kujitokeza  ili wapewe leseni bure za  usafirishaji  vijijini.Na dodoma fm

No comments:

Post a Comment