Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, February 12, 2014

Viongozi wa dini wasema kufungwa kwa misikiti ya Mombasa kunaweza kuchochea siasa kali

 
Wanaume wanaoshukiwa kuwa wanachama wa al-Shabaab wakisikiliza kesi yao katika mahakama ya mwanzo ya Shanzu katika magereza ya Shimo La Tewa tarehe 3 Februari, kufuatia uvamizi wa polisi katika msikiti wa Masjid Mussa huko Mombasa. 
Kamishina wa Kaunti ya Mombasa Nelson Marwa ametishia kufunga misikiti miwili katika jiji hilo-- Masjid Mussa na Masjid Sakina -- kufuatia mapigana baina ya polisi na vijana wa Kiislamu wiki iliyopita.
"Misikiti hiyo ilikuwa ikishukiwa siyo tu inafanya kazi kama sehemu ya kutoa mafunzo lakini pia kama eneo la kuandikisha askari wapya wa magaidi wa al-Shabaab, na njia pekee ya kuwashughulikia ni kuifunga," Marwa aliiambia Sabahi, ingawaje hakubainisha tarehe rasmi ya kufungwa huko.
Viongozi wa dini na wahamasishaji wamepinga mpango wa serikali, hata hivyo, wametahadharisha kwamba kufungwa kwa misiskiti hiyo kunaweza kuongeza kuwafanya vijana kuwa na siasa kali.
"Hizo ni harakati zisizokubalika na zinaweza kuongeza hali hiyo kwa kuwaudhi vijana zaidi na kuimarisha hisia miongoni mwao kwamba serikali iko kinyume nao, hivyo kuwafanya kuwa na siasa kali zaiidi," mjumbe wa kamati ya msikiti wa Jamia wa Nairobi Ibrahim Lethome aliiambia Sabahi.
Lethome alisema kufungwa kwa misikiti kungeweza hasa kuongeza ukiukwaji wa uhuru wa kusali na kunaweza kuonekana kama kutoa adhabu ya jumla kwa ujumla kwa jamii yote ya Waislamu.
Mpango wa serikali "utafanya Waislamu kuona vita vyote hivyo dhidi ya ugaidi kama vinavyolenga isivyo haki Waislamu ambako kutazuia ushirikiano baina ya jamii na serikali", alisema.
Kuepuka msimamo mkali zaidi katika misikiti, Lethome alishauri serikali kutumia upelelezi kubaini kabla matukio yoyote ya uhalifu au shughuli zinazohusiana na ugaidi katika maeneo ya swala.
Viongozi wa Kikiristo na Waislamu waungana
Viongozi wa dini wa Kikiristo pia walipinga kufungwa kwa misikiti.
"Hizo ni harakati za mfarakano ambazo zilishauriwa vibaya na zisizo na tija kwa kuchochea hisia za kidini ambazo zitafanya hali hiyo kuwa ngumu zaidi,"Askofu wa Angalikana wa Dayosisi ya Mombasa Julius Robert Katoi Kalu aliiambia Sabahi.
Kalu alitoa wito kwa serikali kushughulikia suala la ukosefu wa ajira na umaskini katika eneo hilo, ambazo pia ni sababu zinazowasukuma vijana kuingia kwenye siasa kali.
Askafu wa jimbo la askofu mkuu Willybard Lagho alisema kwamba badala ya kufungwa kwa misikiti, serikali, pamoja na viongozi wa dini ya Kiislamu, wangeangalia namna ya kubadilisha udhibiti wa misikiti.
"Msikiti wa Sakina na Mussa ina kamati zake zinazoongozwa na maulamaa ambao mipango yao ni kuingiza ajenda za siasa kali," Lagho aliiambia Sabahi. "Uamuzi wa busara ungeweza kuwa serikali kusaidia kamati hizi kutwaa tena udhibiti wa misikiti hii kuliko kuifunga."
Alilaumu matumizi ya nguvu ya polisi na namna walivyovamia msikiti wa Masjid Mussa, kuingia ndani wakati wakiwa mamevaa viatu vyao, akisema illikuwa kukosa heshima katika nyumba ya kuabudia.
"Mtazamo wa serikali una makosa," Lagho alisema. "Kutumia nguvu nyingi wakati wa kushughulikia matukio haya ya msimamo mkali kunakofanywa na polisi kama tulivyoona wakati wa uvamizi wa Jumapili, wenyewe tu ni msimamo mkali. Serikali inapaswa kuwa na mjadala na kuhusisha jamii, [ambako] tuna uhakika kunaweza kubadilisha hali ilivyo."
Ili kushughulikia msimamo mkali huko Mombasa na sehemu nyingine za nchi, Lagho alitoa wito kwa jumuia ya Waislamu kutafuta wahubiri na wanazuoni wenye msimamo wa kati ambao wanaweza kuhubiri kwa vijana katika misikiti iliyoathirika.
Wito wa uchunguzi, mjadala na suluhisho la kudumu
Siku ya Ijumaa (tarehe 7 Februari) kamati ya kazi inayoundwa na wanazuoni wa Kiislamu tisa na viongozi wa siasa walipelekwa Mombasa katika ujumbe wa kutafuta ukweli wa mambo ili "kujihusisha na viongozi na vijana katika hatua za kushughulikia matatizo yaliyopo katika chanzo cha mgogoro", alisema Seneta wa Mandera Billow Aden Kerrow, ambaye anawakilisha kamati ya kisiasa ya Waislamu na ni mjumbe wa kamati.
"Siku ya Alhamisi, waumini wa Kiislamu, viongozi wa kisiasa na wa umma kutoka Nairobi na Mombasa walikutana katika Msikiti wa Jamia huko Nairobi ili kujadili matukio ya kusikitisha na kujutia katika Msikiti wa Masjid Mussa ambayo yalisababisha mauaji ya watu nane," aliiambia Sabahi.
Kerrow alisema timu itakuwa Mombasa kwa siku tano kabla ya kurejea Nairobi ambako mkutano wa viongozi utaitishwa ili kutangaza matarajio ya baadaye.
"Kwa sasa hatuwezi kukupa maelezo yoyote kuhusu tume ya kutafuta ukweli wa mambo," alisema."Tuko katika hatua ya kujielimisha wenyewe na kile kinachotokea [na] tumeanza hatua za haraka za ujumuishaji ili kuwaunganisha waliotengana na kutoa uongozi muhimu kwa vijana na jamii ya Waislamu kwa ujumla."
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Haki za Binadamu cha Waislamu (MHRF) Al-Amin Kimathi alitoa wito wa uchunguzi huru katika sababu za vurugu za wenye msimamo mkali na unyanyasaji wa polisi ambao umesababisha vifo vya wahubiri na vijana wanaohisiwa kuwa wanachama wa al-Shabaab.
Uanzishaji wa tume ya uchunguzi utasaidia kufichua vyanzo vya vurugu za wenye msimamo mkali na kupendekeza utatuzi wa kudumu, alisema.
"Wakati tunazungumza leo kila mtu, akiwa mtendaji wa serikali au mtendaji wasio wa serikali, ana makosa na anapaswa kulaumiwa kwa kinachoendelea," Kimanthi aliiambia Sabahi. "Ni katika kujitathmini tu kupitia tume huru ya uchunguzi kwamba tunaweza kuliangalia suala hili kwa ujumla ili kutupa msingi wa kweli wa uingiliaji."
"Kwa hiyo, tunataka serikali itoe uchunguzi huru katika sababu za vurugu za kutisha katika Masjid Mussa na maeneo mengine na kutumia hatua zinazokubalika kiraia na kisheria za kutambua na kushughulikia dalili za ukereketwa wenye vurugu kutoka eneo lolote, iwe kidini au isiyo na uhusiano wa dini, watendaji wa serikali au wasio wa serikali," alisema.
Tume ya uchunguzi inapaswa kuongozwa na mtu ambaye ni sawa na jaji wa Mahakama Kuu na ina wajumbe ambao wana utaalamu wa kijamii, kisiasa, kiuchumi na kidini.
Alisema MHRF imedai kuachiwa mara moja kwa watoto ambao walikamatwa katika vurugu na kukamatwa wakati wa uvamizi wa Masjid Mussa. Asasi pia ilitoa wito wa kushtakiwa kwa polisi ambao wanaweza kuwa wamejihusisha katika kutumia nguvu nyingi ambazo zilisababisha vifo na kuumia kwa watu wasio na hatia.
"[Serikali inapaswa] kuahidi na kufungua njia za mjadala na uhusishaji na wote wanaohusika kuleta ukuaji wa hatari wa ukereketwa wenye vurugu katika jamii," Kimanthi alisema.

Chanzo: sabahionline.com

No comments:

Post a Comment