Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, March 28, 2014

KOREA KASKAZINI YAWAAMURU WANAUME WOTE KUNYOA NYWELE KAMA RAIS WAO JONG-UN


 Hii ndio ‘Dear Leader’ style wanayotakiwa kunyoa wanaume wa Korea Kaskazini
Tumekuwa tukisikia sheria mbalimbali zikipitishwa katika nchi mbalimbali zinazowataka watu wavae au wasivae mavazi ya aina fulani, lakini huko Korea Kaskazini imepitishwa sheria inayowataka wanaume wote wa nchi hiyo kunyoa style ya nywele ya kiongozi wao iliyopewa jina la ‘Dear Leader’
Wiki mbili zilizopita serikali ya Korea Kaskazini imepitisha style moja tu ya nywele inayopaswa kufuatwa na wanaume wote ambayo ndio inayopendwa na kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong-Un.
Hapo kabla wanaume wa nchi hiyo walikuwa wanaruhusiwa kuchagua kati ya style 10 za kunyoa zilizokuwa zimepitishwa, lakini sasa ni style moja tu iliyopitishwa, huku wanawake wakiwa wamepewa style 18 za nywele.

SOURCE: MAIL ONLINE

No comments:

Post a Comment