
Mahakama yaahirisha kusikizwa kwa kesi ya Oscar Pistorius.
Kesi ya mwanariadha wa Afrika kusini Oscar Pistorius imeahirishwa baada ya mmoja wa mahakimu kuugua.
Mshindi huyo wa nishani ya dhahabu ya olimpiki , tayari alikuwa amewasili mahakamani ,ambapo alitarajiwa kuwa wa kwanza kujitetea.
Kesi hiyo sasa itaendelea tarehe 7 mwezi Aprili.
Oscar Pistorius amekana kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp kimaksudi lakini anakiri kufyatua risasi zilizomuua akidai kuwa alidhani ni jambazi aliyekuwa ameingia nyumbani mwake.
BOFYA HAPA NA ULIKE PAGE YETU KWA HABARI NYINGIII
No comments:
Post a Comment