Messi
amefunga hat-trick na kuisaidia Barcelona kuiangamiza bila huruma
Osasuna na kupunguza pengo dhidi ya Real Madrid na Atletico Madrid
katika kuelekea taji la La Liga.
Nyota wa Argentina Messi alianza kufungua karamu ya mabao kwa kufunga bao la kwanza kabla ya Alexis Sanchez kufunga bao la pili
Lionel .
Andres Iniesta akafunga bao kwa mkwaju wa yadi 25 na kuifanya Barca kwenda mapumziko wakiwa na mabao 3-0.
Magoli
mawili zaidi ya Messi, na mawili ya Cristian Tello na Pedro,
yaliihakikishia Barca ushindi na kufanya maandalizi makubwa kuelekea
kwenye El Clasico dhidi ya Real Madrid jumapili ijayo.
Mabingwa
watetezi Barca watasafiri hadi Bernabeu kuikabili Real Madrid wakijua
kwamba wanahitaji kuwachapa vinara hao wa La Liga ili kujiweka katika
nafasi nzuri ya kutetea taji lao la La Liga.
Vijana
wa Gerardo Martino wako nyuma ya vinara Real kwa pointi nne na pointi
moja nyuma ya Atletico huku ikibakia michezo 10 kumaliza ligi.
No comments:
Post a Comment