Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, March 21, 2014

Misri yawahukumu kifo wanachama wa Ikhwan

Mahakama ya Misri imewahukumu wanachama 26 wa harakati ya Ikhwaanul Muslimiin ya Misri adhabu ya kifo kwa tuhuma eti za kuvuruga umoja wa kitaifa na kushambulia meli zinazopita katika mfereji wa Suez.
Mahakama hiyo leo imewahukumu wanachama wa harakati hiyo ambao hawakuwepo mahakamani, kwa tuhuma pia za kuanzisha na kuongoza mtandao wa kigaidi. 
 Mahakama hiyo imetangaza kuwa, wanachama hao wa Ikhwaanul Muslimiin watakabiliwa na adhabu ya kifo. 
Mahakama hiyo imemhukumu pia mwanachama mwingine wa harakati hiyo adhabu ya kifungo cha miaka 15 jela. 
Inafaa kuashiria hapa kuwa, jeshi la Misri mwezi Julai mwaka uliopita lilimuondoa madarakani kwa nguvu Muhammad Mursi rais aliyekuwa amechaguliwa na wananchi na kisha kuwatia mbaroni viongozi waandamizi na wanachama kadhaa wa harakati hiyo.
Wakati huohuo, Waziri Mkuu wa serikali ya mpito ya Misri amekutana na Sheikh wa al Azhar kwa shabaha ya kutafuta njia za kukabiliana na fikra za kitakfiri. 

Akizungumza na Sheikh Ahmad Muhammad al Tayeb, Ibrahim Mahlab Waziri Mkuu wa Misri ameisifu nafasi ya al Azhar katika kutoa mafunzo ya Kiislamu na kusisitiza kuwa, Chuo Kikuu cha al Azhar kina uwezo mkubwa wa kukabiliana na vitendo hivyo viovu kutokana na nafasi iliyokuwa nayo ya kimaanawi.

Chanzo: kiswahili.irib.ir

No comments:

Post a Comment