Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, March 2, 2014

MWIGULU AENDELEA KUITESA CHADEMA KALENGA,AVUNA MWENYEKITI CHADEMA KATA YA NZI NA WAFUASI WAKE,AFANYA MIKUTANO MINNE VIJIJI TOFAUTI

 Mh:Mwigulu Nchemba akizungumza na Wananchi wa kijiji cha Mgubika kata ya Nzi wakati wa Mkutano wa kampeni za Ubunge Jimboni Kalenga.Huu ulikuwa Mkutano wa Kwanza katika Mikutano Minne tofauti aliyofanya Mh:mwigulu Nchemba hii leo kata ya Nzi akimnadi Mgombea wa CCM Godfrey William Mgimwa.
 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema kata ya Nzi akijitambulisha Rasmi kwa Wananchi wa Kijiji cha Nzi kuwa yeye ameamua kuachana na Chadema na Kujiunga na CCM kwa hiari yake baada ya kupima Uwezo wa Chadema na CCM kwenye Hoja na Matendo.Mwanachama huyu Mpya wa CCM ameahidi kuongoza timu ya Ushindi kwenye Kata ya Nzi kuhakikisha Godfrey Mgimwa napita kuwa Mbunge.
Pia amesema ataiweka wazi mipango ya Chadema na Watu wageni wa Chadema waliokodishwa na Kupangishwa Nyumba kata ya Nzi wanaotembea Usiku kwaajili ya Kutafuta kura na kushambulia Waoaunga mkono CCM kwenye kata ya Nzi.
Aliyekuwa Mwanachama wa Chadema kutoka kijiji cha Kamiyu na Katibu Mwenezi wa Chadema kata ya Kamiyu akitangaza kuachana na Chadema na Kujiunga na CCM hii leo kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Nzi.
Mmoja wa Wananchama wa Chadema aliyekuwa akisadia kazi ya Uenezi kata ya Nzi akitangaza kuachana nc Chadema na Kujiunga na CCM,Amesema ameamua kufanya maamuzi haya kutokana na Vitendo Vya chadema kuanza kuandaa watu wa Vurugu kwenye Kijiji chake ,Pia Uongoz unaotangazwa na Viongozi wa Chadema kuhusu Kejeli kwa Marehemu Mgimwa eti hakufanya kitu Jimboni Kwake.
Pichani ni Mapokezi kwenye Kijiji cha Kipera jioni ya leo kata ya Nzi.
 

Waliokuwa Viongozi wa Chadema wakimbeba Juu Mgombea wa Chadema wakati anawasili Kijiji cha Kamiyu hii leo wakati wa Mikutano ya Kampeni za Ubunge.

Na.Baraka Kiwango.
Mbio za Kampeni Jimbo la Kalenga zimendelea kushika kasi hii leo,Huku Naibu Katibu Mkuu wa CCM  Bara Mh;Mwigulu Nchemba akiweka kambi kwenye Kata ya Nzi kwa Muda wa masaa 10 na kufanya mikutano Minne siku ya leo kwenye Vijiji vya Kipera,Kimayu,Nzi na Magubika.
Mwigulu Nchemba mbali na Kumnadi Mgombea Wa CCM Kijana Godfrey William Mgimwa,hii leo amevuna Wananchama Viongozi wa Chadema(Mwenyekiti kaya ya Nzi,Katibu Mwenezi na Wanachama 73).Ambao kwa hiari yao wametangaza kujiunga na Chama Cha Mapinduzi wakibeza hatua ya Chadema kuanza kumkejeli Marehemu Mgimwa kuwa hakufanya kitu jimboni kwao ilihali wamefikishiwa Umeme karibia asilimia 80 ya Vijiji vya Kalenga,Amejenga Shule,Vituo Vya Afya na Visima vya maji.Pia haohao Chadema kwenye Msiba walisikika kwenye Vyombo vya habari wakikili kuwa Marehemu Mzee Mgimwa alikuwa kiongozi wa Mfano na Utendaji wake ulitukuka kwa Kalenga na Taifa hili.

Katika hatua Nyingine Mh:Mwigulu Nchemba ameendelea kusisitiza kampeni zifanyike kwa amani na kila chama kina nafasi ya kujenga hoja kuhusu kile watakachokifanya kwe Wanakalenga na sio Matusi.CCM tunajambo la kuzungumza kuhusu Kalenga kwasababu ndio wenye Ilani inayotekelezwa hapa Kalenga na ndio wenye Serikali iliyopo Madarakani,Kinachofanyika hapa ni kumpa kura za ndio Kijana wetu Godfrey Mgimwa akamalizie Utekelezaji wa Ilani ya CCM na Shughuli za Maendeleo alizoacha Marehemu Mgimwa kwa Wanakalenga,Alisema Mwigulu.

No comments:

Post a Comment