Salma Jabu(Nisha) ambaye kwa sasa anakimbiza kwenye sanaa ya uigizaji amefanikiwa kutoa Filamu yake mpya ijulikanayo kwa jina la "GUMZO"Akiwa amewashirikisha wasanii wakongwe na maarufu nchini kama Mzee Majuto,Hemedi Na wengine wengi.Akizungumza na Mtandao wetu wa Dj sek Nisha amesema anashukuru mungu kwa sapoti aliyoipata toka kwa mashabiki wake kwa kuwa toka Movie yake hiyo mpya imeachiwa amefanikiwa kuuza nakala nyingi sana kuliko alivyotarajia,Hivyo kumpelekea kuwa kinara kwa sasa kwenye soko la bongo movie.Filamu ya Gumzo kwa sasa ndio imekuwa Inauzwa kwa wingi kwenye soko la movie toka imetoka na kupelekea kupachikwa jina la malkia wa bongo movie,Utake usitake kwa sasa mwanadada nisha anafanya vizuri sana kwenye uigizaji na sokoni.Filamu hiyo imeshutiwa na director mkali nchini ajulikanaye kwa jina la Kabuti Onyango.
Utamaduni : Rais Samia Atembelea Makumbusho ya Vita vya Majimaji, Songea
Mkoani Ruvuma
-
Matukio mbalimbali wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan alipotembelea Makumbusho ya Vita vya Majimaji, Songea
...
46 minutes ago
No comments:
Post a Comment